Shilole Kugombea Ubunge

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amedaiwa kuwa mbioni kugombea ubunge miaka ya baadae.

Taarifa hiyo imesemwa na msanii wa muziki Bongo fleva  Mr Kesho ambaye amemshirikisha Shilole kwenye wimbo wake mpya ‘Nakudata’, ameweka wazi kuwa mrembo huyo anamipango ya kuwania uongozi kupitia siasa kuongoza wananchi.

download latest music    

Mr Kesho amefunguka hayo Kwenye mahojiano na Bongo 5 ambapo amedai kuwa Shilole sio msanii wa kufanya Muziki maisha yote bali ana mipango mwingine ya kuwa kiongozi:

Kusema ukweli sidhani kama Shilole anaweza kufanya Muziki mpaka miaka mitano mbele mimi nanavyoona ni kama ana ndoto sana za kuwa kiongozi Tena kiongozi wa siasa akaongoza wananchi naweza sema 2020 tunaweza tukamuona Bungeni na mimi namuombea afike huko maana ni mtu Powa sana na ana uthubutu”.

Miaka ya hivi karibuni limekuwa jambo la kawaida kwa wasanii na mastaa mbali mbali kupenda kuingia kwenye mambo ya siasa kwani tumeshawaona wasanii wawili ambao wameshafanikiwa kuingia bungeni ambao ni Mr. Sugu na Profesa Jay Lakini Shilole hajathibitisha taarifa hizi rasmi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.