Shilole: Naepukana na skendo yoyote kwa sasa

Ndoa ya Shilole ambayo itafanyika hivi karibuni imefanya staa huyo kubadili mienendo yake. Shilole sasa ameamua kutulia kuepukana na skendo.

Shilole ameliambia Dimba Jumatano kwamba kwa sasa ameamua kutulia na hatasikika katika skendo yoyote kwasababu anajiheshimu na ameamua kufanya maamuzi hayo kwa moyo mmoja.

download latest music    

Staa huyo pia alidhibitisha kuwa ndoa yake sio propaganda kama baadhi ya watu wanavyodai, alisema kuwa atakua mke wa mtu  hivi karibuni.

“Ndoa yangu si propaganda, mimi ni mchumba wa mtu na niwaambie tu kitu kimoja, nimeamua kutulia na mume wangu mtarajiwa na msitegemee tena kusikia skendo yoyote kutoka kwangu, mara leo kwa Khamis kesho kwa Juma, hapana,” alisema Shilole.

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere