Shilole- Sijapendezwa na Kitendo Cha Uwoya na Dogo Janja Kuachana

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefungukia taarufa za Msanii wa Bongo fleva Dogo Janja na mke Wake staa wa Bongo movie Irene Uwoya kuachana.

Baada ya Uwoya na Dogo Janja kufunga ndoa iliyozungukwa na utata mwaka juzi na kuachana mwaka jana mwishoni hatimaye wawili hao walithibitisha kuachana siku chache zilizopita Baada ya kurushiana maneno ya kejeli kwenye mitandao ya kijamii.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na mtandao wa Dizzim Online, Shilole amefunguka na kuweka wazi masikitiko yake Baada ya kusikia wanandoa hao wameachana ambao pia walihudhuria harusi yake na Uchebe:

Mimi kusema ukweli sijisikii vizuri kabisa kusikia kuwa wameachana hasa kwa sababu haya dini hairuhusu kuachana labda pale inapobidi sanaa Lakini pia huwezi kuingilia maamuzi ya watu.

Unajua kwenye ndoa kuna mengi Mimi na wewe hatuji Lakini wao waliopo humo ndani ndio wanajua nini kinaendelea kwaiyo ni vyema mara nyingi kuwaacha wao wenyewe wanandoa waamue wanachoamua”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.