Shilole: Sina utata rafiki wangu kuwa na mahusiano na wapenzi wangu wa zamani

Zuwena Mohamed maarufu kwa jina la Shilole amefunguka kuhusu ishu ya rafiki zake kuwa na mahusiano na wapenzi wake wa zamani.

Shilole alisema kuwa  mapenzi ni kama ni kama daladala mtu akishuka mwenzake anakaa kwa hivyo yeye hawezi kuwa na uchungu rafiki zake wakipendana na wapenzi wake wa kitambo.

download latest music    

Staa huyo pia alifunguka na kusema kuwa atafunga ndoa wakati wowote kwani mpenzi wake tayari ameshatoa hela ya barua.

“Mimi kwa sasa hivi sina boyfriend kabisa, niwaambie tu nina mchumba ambaye tayari ameshanitolea mpaka barua, Mungu akijaalia harusi nitawakaribisha siku siyo nyingi. Na kuhusu wapenzi waliopita kuwa na mahusiano na marafiki zangu naona ni kitu cha kawaida kwa sababu naamini mapenzi ni kama daladala ukishuka mwenzako anakaa” Shishi alikiambia kipindi cha 5Selekt ya EATV.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere