Shilole: Siwezi Kumpiga Uchebe Hayo ni Mapenzi ya Kitoto

Mwanamuziki wa Bongo fleva Shilole amefunguka na kusema kwenye ndoa yake na Uchebe hawana drama zozote hasa mambo ya kumpiga makofi hawezi kwa sababu Uchebe ni gentleman.

Shilole aliwashtua watu wengi ikiwemo familia yake baada ya kufunga ndoa ya siri iliyohudhuriwa na watu wasiopungua kumi tu nyumbani kwa Babu Tale usiku usiku huku baadhi ya ndugu zake kuonyesha wazi kutofurahishwa na jambo hilo.

download latest music    

Lakini tangu afunge ndoa Shilole amewashangaza wengi kwa ukimya kutawala kwani Kumekuwa na drama nyingi katika mahusiano mengi ya nyuma ya Shilole kwaiyo hali ya ukimya miezi yote hii ni hali ya kushangaza kidogo.

Lakini pia habari za Shilole kuwa mbabe na kuwachapa makofi wapenzi wake sio suala geni kwa mashabiki zake na baada ya kufunga ndoa na Uchebe wengi walikuwa wanasubiria siku Uchebe apigwe makofi ya nguvu na Shilole.

Lakini kwenye Interview aliyofanya na Enews ya East Africa Tv, Shilole amekiri kuwa tabia hiyo ameiacha na ilikuwa ni utoto tu fununu kuwa Uchebe ni kiburi na mkorofi zaidi yake Shilole amelieleza hapa:

Mume wangu ni like gentleman ni mwanaume ambaye ana msimamo mtu akiwa na msimamo kama hujamjua unaweza kusema ana kiburi alafu mimi nilishamjulia mume wangu anapenda nini na yeye alishajua ninapenda nini kwaiyo mambo yanaenda vizuri. Halafu suala la kumpiga makofi kwa Uchebe siwezi pale inakuwa ngumu mwenyewe unamuona yule alikuwa anapigana ana mkanda yule lakini nikimpiga nampiga makofi ya chumbani tu ya kimahaba kaniruhusu mwenyewe lakini kupigana ngumi na mume wangu haitotokea”.

Lakini pia Shilole amesisitiza kuwa tabia yake ya kupiga wanaume ilikuwa zamani ambayo ni tabia ya kitoto aliyokuwa anafanya lakini hivi sasa amekuwa hivyo hawezi kunyanyua mkono wake na kumpiga mumewe na mumewe hawezi kumpiga.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.