Shiloleh Ajipanga Kurudi Shule Tena.
Mwanadada na msanii maarufu zuwena mohamed ambae siu chache zilizopita alikuwa amepata nafasi ya kwenda kutembelea chuo cha NCT ambapo alipata nafasi pia ya kuona kozi mbalimbali zinazopatikana chuon hapo na kuongea na baadhi ya wanafunzi alifunguka na kuhaidi kuwa atajipanga na yeye kurudi chuoni hapo kwa ajili ya kuongeza elimu kuhuusu mapishi.
Shiloleh ambae ukiachana na kazi ya muziki anayoifanya lakini pa ni mpishi mzuri wa chakula na amekuwa akiwalisha watu wengi jijini, amesema kuwa kuna haja ya yeye kurudi chuo na kusomea kozi hiyo ili kuongeza ujuzi zaidi.
kutoka katika chuo cha NCT waliandika haya baada ya shishi kuondoka chuoni hapo” siri imefichuliwa na shishi mwenyewe mmiliki wa mgahawa wa shishi food kuwa kumbe mambo yanalipa sana , ila yeye hakusita kufika chuoni hapa NCT kuiongezea thamani ya chakula chke kwa kupata dondoo juu ya ukarimu na ufahamu kuhusu ujasiriamali lakini pia utaalamu katika maswala ya food production.
alisema kuwa atakuja yeye na team yake kupata kozi fupi , ulikuwa ni wakati mzuri kukutana na anayeitumikia sekta ya ukarimu wake na wale wanaojiandaa nafasi bado ni nyingi , hataki ujinga wa kupishana na fursa.aante sana shishi kwa kupata nafasi ya kutembelea hapa.
Shiloleh anawekwa katika list ya wasanii wanaojituma na kufanya kazi buoa kukata tamaa hasa kutokana na kuamua kufanya muziki na mapishi kwa wakati mmoja.