Shiloleh Amtupia Bango Diamond Kuhusu Tetesi za Kulogwa na Wanawake.
Ikiwa katika mitandao ya kijamii kumekuwa na habari za kuwa mwanamuziki Diamond Platinumz amekuwa akilogwa na mama wa mtoto wake mdogo anaejulikana kama Hamisa Mobeto, habari ambayo ime-trend sana ktaika mitandao wikiend hii na wiki hii yote kwa ujumla mwanadada shiloleh nae ameamua kupigilia msumari wa moto kutoka katika habari hiyo.
Katika ukurasa wake wa instagram, Shiloleh aliandika baada ya kuweka picha ya Diamond Platinumz huku akimtania kuwa muonekano wake mpya unavutia kufuatia kusuka kwake nywele huku akisema kuwa na ndio maana wanawake wamekuwa wakimloga.”kakangu diamond umedamshi na ndio maana wanawake wanakuloga”
Hata hivyo tangu kumesambaa kwa maneno hayo katika mitandao ya kijamii mwanadada Hamisa Mobeto hajataka kuongea kitu kuhusu hilo zaidi ya kuonyesha shughuli zake zikiendelea kufanikiwa.