Show Za Diamond Zinajazwa na Wazungu na Wajamaica Sio Waafrika Pekee- Babu Tale

Meneja wa staa wa Muziki wa Bongo fleva nchini Diamond Platnumz, Babu Tale amefunguka na kueleza hali ya shoo za Diamond kwenye Tour ya ‘A boy from Tandale’ inayofanyika nchini Marekani.

Babu Tale amefunguka na kuweka wazi kuwa katika shoo zinazoendelea kufanyika nchini Marekani kwa sasa zinakuwa zinahudhuriwa na mashabiki wa mataifa mbali mbali kama wazungu na sio Waafrika tu kama ilivyozoeleka.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na JJ wa Jembe FM Babu Tale ambaye ameongozana na Diamond katika tour hiyo, amesema kuwa show za Diamond zimekuwa ni za watu wote na si wale kutokea Afrika pekee.

Ukiangalia clip ambayo ameposti Diamond utaona watu weupe kibao, nimeona wazungu kibao, Jamaica walikuwepo“.

Imekuwa ni Kasumba kuwa wasanii wanaoenda kufanya shoo nje ya nchi huishia kupiga shoo za sebuleni jambo ambalo Diamond amekuwa akilibadilisha kwani amekuwa akionekana akipiga shoo Kwenye kumbi kubwa na kujaza mashabiki kibao.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.