Sifanyi Shoo Mwezi wa Ramadhan;-Tunda Man
Msanii Tunda Man amefunguka na kusema kuwa mwezi huu mtukufu wa ramadhani ni mwezi wa toba na sala hivyo hata siku moja katika mwezi huu hawezi kufanya kazi yoyote ya sanaa kwa sababu muda mwingi anakuwa katika swala.
Tunda Man anasema hiki ndicho kipindi cha kufanya toba na kumrudia Mwenyezi Mungu na pia kumshukuru kwa kila kitu .
Mimi mwezi huu mtukufu huwa naacha kila kitu, hata mtu aje na show ya milioni mia 2 sifanyi shoo, na nina swali sala zote tani ilimradi tu nimtumikie mwenyezi Mungu anisamehe madhambi yote niliyoyafanya.
Hata hivyo Tunda Man anasema kuwa kesi inayomkabili babu tale kwa sasa haimuhusu bali ilitakiwa kuwa ya Abdul Bonge lakini Abdul Bonge hayupo
Ile kesi haimuhusu kabisa Babu Tale , ile kesi ilikuwa ya abdul bonge na Abdul Bonge ni marehemu sasa, kwa kuwa wale ni tip top connection basi ile kesi hata mimi inanihusu.