Sijawahi Kufikiria Kuishi Maisha Haya -Harmonize.
Msanii wa muziki wa bongo fleva nchini kutoka katika kundi la wcb, Harmonize amefunguka na kusema kuwa katika maisha yake hakuwahi kuwaza kusihi maisha kama anayoishi sasa hivi ambavyo alivyokuwa akiishi maisha magumu na maisha mazuri aliyonayo sasa.
Harmonize amefunguka na kusema kuwa miaka mitano aliyokuwa nayo huko nyuma hakuwahi kuwaza kuwa kama leo kutokana na kwamba alikuwa tu anafanya biashara ndogondogo,
miaka mitano iliyopita nilikuwa ninafanya baishara ndogo ndogo hapa hapa kariakoo,nilikuwa machinga mwenye shida, tabu , suluba nilizokuwa napitia kila siku.mungu mwenyewe ndio alikuwa anajua , hata ukiangalia 90% ya wimbo wangu wa matatizo ilikuwa ni maisha yangu ya nyuma.sina utajiri wowote lakini kwa afadhali niliyoipata naona mwenye bahai sana.
Maisha ninayoishi sikuwahi kufikiria kama nitaweza lakini pia nina mshukuru mungu kwa kunipa nafasi ya kukumbuka ndugu zangu niliyowaacha maeneo haya.