Sijawahi Kuumia Kisa Mapenzi, Nina Foleni ya Wanaume: Wolper

Muiguzaji mashuhuri wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Jacqueline Wolper amefunguka na kusema hajawahi kuumizwa na mapenzi hata siku moja kwani kuna wanaume wamepanga foleni.

Wolper ambaye mwaka jana alikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na msanii kutoka WCB Harmonize lakini waliachana na baadae akaingia kwenye mahusiano na mwanamitindo Brown kisha naye akaachana naye ndipo inasemekana hivi sasa anatoka na msanii anayeitwa Engine.

download latest music    

Wolper amefunguka na kusema kuwa hajawahi kulia kisa mapenzi bali kinachomuumizaga akiachana na mtu ni kwa sababu tu ametangaza na si vinginevyo kwani kuna kuwaga na msururu na foleni ya wanaume wanaokuwa wanamhitaji muda wowote.

Wolper amefunguka hayo kwenye mahojiano aliyofanya na Global Tv alipohudhuria baby shower ya Gigy Money siku ya Jumamosi iliyopita:

Sijawahi kuumizwa na mapenzi yaani nisikufiche kabisa sijawahi kuumia kuachana na mtu ila naumia kwa nini nilimtangaza kuachana kuumia hapana kwanza kwa sababu nina foleni ya wanaume wamejipanga wananisubiri nitoke kwenye Mahusiano kwaiyo mimi ndio ninachagua nimchukue nani”.

Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa kwa sasa anaelekeza nguvu zake zote kwenye biashara yake ya nguo na filamu ataweka kando kwa sasa kwani anataka biashara yake imfikishe mbali.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.