Siku Zote Mtu Utafuta Kile Kisichoonekana:-Shusho Aongea na Wasichana.

Mwanamuziki wa nyimbo za injili nchini, Christina Shusho amefunguka na kuwahasa wanawake hasa wasichana wa kileo ambao wamekuwa wakizoe kuweka miili yao wazi na kupiga picha zinazoonyesha maungo yao kuwa yako wazi kuwa hakuna mtu anaetamani  vitu hivyo.

Mwanamuziki huyo amesema kuwa wanatakiwa kujua kuwa kila siku kinachoafutwa ni kile kisichoonekana kwaio kama unaweka mwili wako wazi ni vigumu watu kuvutiwa nawe kwa sababu wanajua kila kitu kuhusu wewe.

download latest music    

Siri kubwa ninayotaka kuwaambia wadada ni kuwa siku zote unapoficha mwili wako ndio unazidi kuvutia,  na kufanya watu wakutamani.Maana siku zote mtu huwa anatafuta kile kischooneka na wala sio vilivyo wazi na unapovaa nguo za ajabu unaondoa thamani yako.Maana hakuna mwanaume anyeweza kuja tu na kuokota kimgomba ambacho kiko hapo tu , na hata kama atakuja atakuwa anakudanganya tu lakini in reality anaondoka na kutafuta yule anaejihifadhi.

 

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.