Simchukiii Hamisa ila Nampenda Sana Wema. :-Diana Kmary
Mwanadada Diana Kimary amefunguka na kusema kuwa anapinga vikali maneno yanayosemwa katika mitandao kuwa yeye hana bifu na Hamisa Mobeto kwa sababu tu yuko karibu na Wema ambae kwa sasa amekuwa kama adui wa Hamisa kutokana na figisu za hapa na pale.
Diana anasema kuwa watu wanaofikiria hivyo wanapaswa kujua kuwa kila kitu anachoweka aktika itandao ya kijamii hakina lengo la kumlenga mtu yoyote kama wanavyosema kuwa vitu hivyo vinamlenga Hamisa.
Simchukii wala sina bifu na Hamisa kama watu wanavyotengeneza katika mitandao ya kijamii,bali wakiona kuwa nina muweka wema wajue tu kuwa nina mapenzi kama yote, na hata kama ninaandika ujumbe sio kwamba nina msema mtu.
Mwanadada huyo ambae mpaka amechora tatoo ya jina la Wema katika paja lake kuonyesha kuwa ni jinsi gani amekuwa na mapenzi na Wema Sepetu.