Simuoni wa Kunipa Upinzani :-Fid Q
Rapper mkongwe nchini fareed kubanda maarufu kama Fid Q amefunguka na kusema kuwa kitu kikubwa kinachsababisha wasanii wengi na kazi zao kushindwa kufanya vizuri ni kutokana na upinzani mkubwa wanaotengeneza baina yao na kuweka mashindano sana.
Maswala ya mashindano mara nyingi mimi huwa siyapendi sana kwa sababu huwa yanatengeneza majkundi na ma-timu mabvyo vinawadumaza wasanii wakashindwa kufikiria jinsi ya kukuza muziki wao, badala yake wanakuwa wanafanya muziki kwa ajili ya kupata nafasi kwa mashabiki badala ya kufanya muziki mzuri.
Fid q anasema kuwa swala hilo la upinzani linafanya kiasi kwamba wasanii wapya wanaokuja wanaokuwa hawapati attention kubwa kwa mashabiki kwa sababu tu wanakuwa tayari wametengeneza upinzani wa Simba na Yanga.
hata hivyo fid q anasema kuwa kwa upande wake hana shida na wala hana mpinzani kwa sababu muziki wa aina yake hakuna wa kufanana nae.
mimi binafsi sina chalenge kwa sababu nimekuwa nikifanya muziki wangu kwa muda mrefu na wala sina mpinzani wa kushindana nae.