“Sina Bifu na Mobetto Lakini Nampenda Wema”-Diana Kimary

Muigizaji wa Bongo movie Diana Kimary amefunguka na kudai hana bifu wala hamchukii Hamisa Mobetto ila tu anampenda sana Wema Sepetu.

Diana Kimary ambaye siku za hivi karibuni ameonekana kuwa na Ukaribu sana na Wema ameweka wazi kuwa watu wengi wanadhani yeye ana bifu na Mobetto kwa sababu yuko na Wema jambo hilo sio la kweli.

download latest music    

Kwenye mahojiano na gazeti la  Ijumaa Wikienda, Diana ambaye hivi sasa yupo karibu na Wema alisema watu wengi wanajua ana bifu na Mobeto, lakini wanashindwa kuelewa anapoweka vitu vyake kwenye mtandao wake wa kijamii wa Instagram havilengi kumsema mtu.

Simchukii na wala sina tatizo na Hamisa (Mobeto)kama watu wanavyotengeneza kwenye mitandao, bali wakiona namuweka Wema ni kwa vile nina mapenzi kama yote kwake pia hata nikiandika ujumbe simsemi mtu”.

Wema na Mobetto wametajwa kuingia katika bifu zito kwa sababu ya Jina la ‘Tanzania Sweetheart’ ambapo mashabiki wamedai wamemvua Jina hilo Wema na kumvalisha Mobetto jambo ambalo Wema amepingana nalo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.