“Sina Mpango wa Kuolewa Ndio Maana Nimezaa Nje ya Ndoa Mapema”- Hamisa

Muigizaji wa Bongo movie na mwanamitindo maarufu Hamisa Mobetto ambaye pia ni ‘babymama’ au mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz Amefunguka na kukiri kuwa hajafikiria na wala hana mpango wa kuolewa kwa hivi sasa.

Hamisa ambaye alikamata headlines mwaka jana kwa kuwa mchepuko wa Diamond kwa miaka Tisa na hatimaye kuzaa naye mtoto wa kiume anayeitwa Dylan. Lakini tangu aseme ukweli kuhusu mahusiano yake na Diamond wamekuwa hawana maelewano mpaka jana walipopatanishwa mahakamani.

download latest music    

Hamisa ana umri wa miaka 24 lakini katika umri wake mdogo amejaliwa kupata watoto wawili ambao mmoja ndio Dylan aliyezaa na Diamond na mwingine ni Fantansy aliyezaa na mkurugenzi wa Efm Majey au Majizzo.

Siku ya jana Hamisa alipokuwa anatoka mahakamani kusikiliza kesi ya madai ya malezi ya mtoto aliyemfungulia mzazi mwenzake Diamond katika mahakama ya watoto Kisutu alifunguka na kusema hana mpango wa kuolewa tena na yeye ni mtu ambaye haamini katika ndoa.

Kusema kweli sina mpango wa kuolewa any time soon yaani kabisa kabisa am not ready siko tayari kufunga ndoa kabisa kwa hivi sasa lambda ikitokea mbeleni huwezi jua lakini mimi ni moja kati ya wale watu ambao hawaamini kuhusu kufunga ndoa ndio maana unaniona nimezaa watoto nje ya ndoa mapema kabisa”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.