“Sina Sababu ya Kusema Namuhurumia Kapata Matatizo Shauri Zake”. Amefunguka Faiza Baada ya Sugu Kufungwa

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara Faiza Ally ambaye amejipatia umaarufu zaidi kutokana na kuwa mzazi mwenza wa Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’.

Uhusiano wa Sugu na Faiza sio mzuri siku zote kwani ni mara nyingi wamekuwa watu wa kurushiana maneno Kwenye mitandao ya kijamii huku Faiza akimtuhumu Sugu kwa kukataa kumlea mtoto wao na kupelekea vita kali kati yao.

download latest music    

Siku ya Jumatatu Sugu alihukumiwa kifungo cha miezi mitano Jela baada ya kukutwa na hatia na mahakama ya hakimu mkazi Mbeya ambapo Sugu alihukumiwa kwa kudaiwa kutoa maneno ya uchochezi na lugha ya fedheha dhidi ya raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. J.P Magufuli.

Baada ya hukumu hiyo hatimaye mzazi mwenza wa Sugu, Faiza amefunguka kuhusiana na hukumu hiyo na kusema amechukizwa na kitendo hicho kilichofanyika maana hakikuwa cha haki kabisa.

Faiza amesema hayo kwenye mahojiano aliyofanya na Radio 5 ambapo amedai kitendo hicho kimemuuma kama mzazi mwenzake ingawaje maisha yake yanakuwaga magumu zaidi Sugu akiwa uraiani.

Nikimuangalia kwenye maisha yangu namuona kama adui ambaye hana neno kwangu, kwaiyo mimi sina sababu ya kusema sijui namuhurumia sijui kapata matatizo shauri zake, Hayo matatizo kwa kweli naona akiwa uraiani maisha yangu yanakuwa magumu sana, sijali japo siombi akae jela hivyo lakini saa nyingine naona inabidi aah sijali kwa kweli”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.