“Sina Ujauzito Bali Nimenenepa Kwa Raha Za Mume Wangu”- Shilole

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kwa jina la usanii kama Shilole amekana Tetesi za kuwa yeye ni mjamzito na kudai amenenepeana kwa sababu ya raha za ndoa.

Tetesi za Shilole kuwa mjamzito zimekuwa zikishika kasi tangu Afunge ndoa ya ghafla na mume wake Uchebe mwaka jana mwishoni.

download latest music    

Na taarifa hizo zinatokana na kiukweli Shilole amenenepa sana na kujiachia mwili wake kiasi ya kwamba kuwa na mwili mkubwa tofauti na alivyokuwa siku za nyuma.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Shilole alisema kuwa, amenenepa kwa ajili ya raha anazopewa na mumewe Uchebe na kuridhika na maisha yake, lakini siyo kwamba ana ujauzito.

Watu wengi wanasema hivyo, lakini mimi sina ujauzito, bali nimenenepa tu kwa raha anazonipa mume wangu,” alisema Shilole na kudai kwamba, wanaosema hivyo siyo watu wabaya kwani wanamtakia heri na mambo mazuri“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.