“Sio mbaya mkiniita Gigy Dangote” Gigy aeleza anavyompenda Diamond Platnumz

Gigy Money ambaye ni video vixen mkubwa kutoka Tanzania amewaacha wengi wakijiuliza uhusiano wake na Diamond Platnumz ni upi baada ya yeye kuweka picha yake akiwa na CEO huyo wa Wasafi records huku akiandika kusema anavyompenda.

Mwana dada huyu ambaye amefanya kazi na wasanii kama Harmonize hata hivyo hakuwa na nafasi ya kuwajibu mashabiki wake ambai walitaka kujua kama alikuwa anammezea msanii huyu.

download latest music    

Kupitia mtandao wake wa Instagram, Gigy aliandika kusema…

Nampenda sana Chibu sio kwamba ajui ?ila sio mbaya mkiniita gigy dangote❤ amen? #ilatunapendezana @diamondplatnumz

Mashabiki wengine waliacha majibu ya kumponda mrembo huyu wakimfananisha na Zari Hassan huku wengine wakimwabia mtu anayemfaa sana ni Harmorapa. Tazama picha hiyo hapa chini.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua