Sihofii Kuibiwa Uchebe, Namwamini Sana-Shilole Kaongea

Ingawa ni moja wa wasanii waliosemwa sana katika mitandao kuhusu tabia yake ya kutembea na wanaume wanaowazidi umri, Shilole hajawahi kukoma kufanya hivyo huku akisema kuwa yeye kwake anachoamini ni mapenzi na sio kitu kingine na swala la umri linabaki kuwa namba tu,Shilole ambae anasifiika kwa tabia ya kuwa na mahusiano na wanaume wadogo lakini pia ikisemekana kuwa amekuwa akiwaonea sana hata kuwapiga muda mwingine amefunguka na kusema kuwa mpenzi wake alienae sasa hivi anamuamini sana hivyo wala hana wasiwasi nae.

” Sihofii kabisa kuibiwa uchebe wangu maana ninamwamini sana, na yeye ananiamini sana hata ninpokuwa safarini  nje ya nchi huwa sina hofu yoyote maana ni mtu wa dini sana mume wangu  na huwa hana hayo mambo ya wanawake” Alizungumza shilole.

download latest music    

Shilole aliendelea kumsifia mpenzi wake huyo huku akisema kuwa kwa upande wao mapenzi yao huwa wanayatamguliza kwa Mungu , ndio maan awanaweza kukaa kwa amani kabisa maana bila kumshirikisha Mungu katika ilo hakuna kinachoweza kufanyika  kwa akili zao katika hilo,”mapenzi yetu tunamtanguliza Mungu zaidi  maana kwa akili zetu hatuwezi.”

Shilole na Uchebe wamekuwa katika mahusiano kwa takribani miezi kadhaa sasa imepita lakini, mwanaume huyo alienae iliwahi kusemekana kuwa alikuwa mume wa mtu wa ndoa lakini alipoingia katika mahusiano ya kimapenzi na shilole aliamua kumuacha mke wake kwa talaka kwa ajili ya kukaa na Shilole ambae pia inasemekana kuwa huwa akiwapa ela wanaume hao ili waendelee kukaa nae.

Ukiachana na Uchebe, Shilole pia alishawahi kuwa na mahusiano na msanii mwenzie, Nuh Mziwanda kwa kipindi cha nyuma lakini walipokuja kuachana Nuh Mziwanda alifunguka na kusema kuwa Shilole alikuwa alimuonea sana na kumfanya kama mtoto kwa sababu tu alikuwa akimzidi ela na umri pia, kwa kifupi Shilole anasemekana kuwa ni wamama wenye tabia ya kulelea wanaume ivyo ujiingiza kwenye mahusiano wa wanaume wenye umri mdogo ili aweze kuwamudu na kuwaendesha vile anavyotaka yeye.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.