Siri anayotumia Ray C kunoa makali yake kimuziki itakushangaza sana

Ray C ameachana na mambo ya kutumia dawa za kulevya kabisa, kwa sasa akili yake yote iko tu kwa mambo ya muziki pekee.

Mrembo huyo alifunguka na kusema kuwa hana hamu na mambo ya mapenzi kwasababu ya malengo yake kimuziki.

download latest music    

Soma pia: Ray C atoa sababu ya yeye kuwa single

T Fighter, mmoja wa mameneja wa Ray C, pia amefunguka kuhusu siri ambayo mrembo huyo anatumia kunoa makali yake kimuziki.

Akiongea na Planet Bongo ya EA Radio, T Fighter alisema Ray C ako na uwezo wa ajabu kwani yeye hushinda studio kwa siku mbili mfululizo akirekodi ngoma zake.

“Tukienda studio tunakesha hata siku mbili, mimi nishazoea nikienda studio nakaa lisaa limoja naondoka ila yeye akiingia studio anakaa siku mbili anarekodi nyimbo tatu au nne kali,” T Fighter alisema.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere