Siwezi Kujichubua Naipenda Rangi Yangu-Vanessa Mdee

Msanii wa Bongo fleva anayefanya vizuri kitaifa na kimataifa Vanessa Mdee amedai kuwa hatokaa ajichubue rangi yake ya mwili na haamini kwenye kujibua.

Kumekuwa na kasumba kubwa ya wasanii kujibalisha rangi ya mwili kwa kudhani kuwa ndio wanakuwa warembo zaidi, huku wasanii wengi wa mziki na filamu wamenyooshewa vidole na kudhaniwa kuwa wanajichubua.

download latest music    

Katika mahojiano aliyoyafanya hivi karibuni Vanessa alifunguka kuhusiana na msimamo wake juu ya swala zima la kujichubua ambapo alisema;

“Mimi kama Vanessa siamini kwenye kujikoboa, kujichubua au kujibadilisha rangi yako ya kawaida au mwili wako wa kawaida my belief is in temporary stuff, so ukaweka make up au nywele ukuongezea hiyo ni kitu temporary ambayo usiku ukiamua unatoa lakini vile vitu vya kufanya moja kwa moja siviamini”.

Pia Vanessa aliongezea kuwa;

“Na pia ile issue ya confidence, mtu ukiwa secured unaweza kufanya hivyo vitu ukiwa unataka kujiboresha au kujiridhisha mwenyewe ukadhani ukijibadilisha utakuwa bora zaidi but I don’t think I need to do that“.

Vanessa ameongeza kuwa hawezi kufanya hivyo kwasababu ni kinyume na maadili yake ya kidini na dini imekataza kufanya hayo anachofanya yeye ni kumshukuru Mungu kwa kumfikisha hapo alipo leo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.