“Siwezi kumfurahisha kila mtu” Linah awajibu wanaotaka afunike tumbo lake

Image: Linah

Linah ambaye anamtarajia mtoto wake wa kwanza hivi karibuni ameamua kuwajibu mashabiki ambao wameonesha kuwa na shida na picha ambazo aliweka kwenye mtandao wake wa Instagram kuonesha tumbo lake.

Msanii huyu wa Bongo alisema haya baada ya mashabiki kadhaa kuacha maoni ambayo yalikuwa ya kuudhi kwenye picha zake ambazo aliweza kuonesha ujauzito wake.

download latest music    
Linah aonesha Ujauzito wake
Linah aonesha Ujauzito wake

Hata hivyo Linah haoni ubaya wa picha hizi na ndio maana amewajibu mashabiki hawa. Kulingana na alichosema, Linah haoni kwamba anaweza kufurahisha kila mtu na kwa upande wake haoni kama kuna shida yoyote.

“Siwezi kumfurahisha kila mmoja ndio maana anafanya kile ambacho anahisi kipo sahihi kwa upande wangu pia wakosoaji wapo wengi tu”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua