Siwezi Kuwa Video Queen- Lulu

Msanii mkongwe wa Bongo movie Mrembo Elizabeth Michael amefunguka na kudai hawezi kuwa mtumwa wa pesa kwa kufanya kila kazi iliyopo mbele yake.

Lulu ambaye alijipatia umaarufu tangu akiwa na miaka nane Kupitia uigizaji amefunguka na kudai hawezi kutaka kufanya kila sanaa kwa sababu tu ni msanii bali ameridhika kuwa muigizaji basi.

download latest music    

Lulu aneweka wazi kuwa tofauti na wasanii wengi wa Bongo movie yeye binafsi hawezi kabisa kufanya kazi kama video queen Kwenye video mbali mbali za wasanii.

Nadhani kwa kiwango nilichofika ni wakati wa kushika hiki hiki, siwezi kuwa Video Queen na Actress. Siwezi kuwa mtumwa wa pesa kwa kufanya hivyo Some times ni kuweka tu mipaka ya kazi zako”.

Anasema kama ni suala la kupata kwa njia ya sanaa, uigizaji unatosha na anafikiria anahitaji kujikita zaidi huko kuliko fani nyingine, kwani anaamini ameandikiwa kupata kupitia huko na si kuhangaika huku na huko akiendekeza pesa na anaamini bila kuwa na msimamo ni rahisi kufanya hata kazi mbaya.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.