Solo Thang Akiri Kuzimika na Maua Sama

Msanii mkongwe wa Muziki wa Bongo fleva aliyetamba kwa miondoko yake ya kuchana miaka hiyo Msafiri Kondo maarufu kama Solo Thang amefunguka na kukiri kumkubali msanii mwenzake Maua Sama.

Solo Thang ambaye amekuwa kimya kwa miaka mingi baada ya kuhamia nchini Uongereza amekiri bado anafuatilia kwa ukaribu Bongo fleva na msanii wa kike anayemkuna ni Maua Sama.

download latest music    
Solo Thang

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Solo Thang amesema katika wasanii wa kike Maua ndio anajua muziki pia ni miongoni mwa wadada wa Bongo fleva wanaomkuna sana.

Kiukweli ninapenda anachokifanya Maua Sama, ni mwanamuziki mzuri, ingawa nipo nje namsikiliza sana na anasikilizwa sana pia, lakini mbali na yeye wanamuziki wengine kama Diamond, Ally Kiba, A.Y, Fid Q, kazi zao zinatufikia na tunapata nafasi ya kuzisikiliza“.

Maua Sama anafanya vizuri na wimbo wake unaoitwa Amen aliomshirikisha mkali wa RnB Ben Paul.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.