Soudy Brown na Maua Sama Watiwa Mbaroni

Mtangazaji wa kipindi cha Shilawadu cha Clouds Tv, Soudy Brown na msanii wa Bongo fleva anayefanya vyema na ngoma yake ya ‘Iokote’ wamekuwa mbaroni mapema jana.

Soudy Brown na Maua Sama wanadaiwa kukamatwa na Polisi Kinondoni lakini mpaka jana jioni tayari walikuwa wameshahamishiwa Central Polisi.

download latest music    

Bongo 5 wanaripoti kuwa wawili hao walishikwa siku ya jana baada ya kupost video mtandaoni inayowaonekana watu wakicheza wimbo ‘Iokote’ wa Maua Sama huku wakiwa wanakanyaga hela.

Kamanda wa polisi kanda maalumu Dar, Mambosasa amefunguka na kuweka wazi kuwa Polisi inamshikiria mtangazaji Soudy Brown na mwanamuziki Maua Sama  kwa kosa la uharibifu wa mali. Inadaiwa wameonekana mtandaoni wakirusha hela na kuzikanyaga jambo ambalo ni kinyume na sheria.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.