Stamina Ahaidi Kumtembezea Kichapo Msanii Huyu

Mwanamuziki wa Hip hop ya Bongo fleva Stamina amefunguka na kumjia juu msanii anayejulikana kwa jina la Edu Boy na kuahidi kuwa sehemu yoyote ayakayomkuta ni lazima atampa kipigo heavy.

Edu Boy ambaye anafanya mziki wa Bongo fleva alitoka na ngoma yake ya Bongo fleva inayojulikana kama ‘tunasafisha’ aliyowashirikisha Amber Lulu na Belle 8 ambapo ndani ya ngoma hiyo aliwadiss wasanii kama Dogo Janja na Stamina.

download latest music    

Baada ya Stamina kusikia wimbo huo alianza kwa kuwablock wasanii wote walioshiriki kwenye ngoma hiyo kuanzia Edu Boy mpaka Amber Lulu na Belle 9 lakini pia Stamina alimpa ujumbe EduBoy kuwa ajifiche asikutane naye kwani akikutana naye tu lazima amtembezee kipigo cha miezi.

Edu Boy amefunguka na kusema hamuogopi Stamina wala nini na ana uhakika hata akikutana naye sehemu yoyote hawezi kumfanya chochote.

Kwenye mahojiano yake na Bongo 5 alifunguka na kusema:

Siishi chini ya Sheria ya mtu naishi chini ya sheria ya nchi ila siishi kama nikimchana Stamina nitakutana naye anipige, kwanza naamini hana uwezo wa kukutana na mimi akanipiga naamini kwa asilimia mia”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.