Steve Nyerere Adai Kutishiwa Kuuawa na watu Wasiojulikana.

Msanii wa bongo movies Steve Nyerere amefunguka na kusema kuwa kuna watu wasiojulikana wamekuwa wakimtishai kumuu a hivi karibuni, na ni watu ambao wanaonekna kuyafatilia maisha yke na kuyajua kiundani  zaidi.

Steve Nyerere anasema kuwa amekuwa na maisa ya wasiwasi na kuwa kama yatima kwa sababu kuna watu wamekuwa wakija mpaka nyumbani wakimtafauta na hata kumtumia meseji za vitisho katika simu yake.

download latest music    

Steve Nyerere anasema kuwa amekuwa na maisha ya wasiwasi na wala hajui kesho yake lakini kitu kikubwa amekuwa akiwaza sana juu ya familia yake tena hasa watoto wake ambao bado wamekuwa wakimuhitaji sana.

Steve anasema kuwa amekuwa akiipenda sana Tanzania na anachoamini kuwa hata hao wanaofanya hivyo wanamjengea ujasiri wa kujiamini na kupambana pia.

Steve amekuwa moja ya msanii anaekumbana na upinzani hata kutoka kwa wasanii wenzake mara nyingi kutokana na sababu mbalimbali na hata kufikia hatau ya kuwa wakirushiana maneno katika mitandao ya kijamii.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.