Steve Nyerere Amtaja JB Kuwa ‘Bodyguard’ Wake

Muigizaji wa Bongo movie ambaye amebobea kwenye kuingia sauti za viongozi mbali mbali wa siasa Steve Nyerere ameibuka na jipya hivi karibuni Baada ya kudai msanii mwenzake JB ni mlinzi wake.

Gazeti lab ijumaa linaripoti kuwa Tukio hilo lilijiri katika Hoteli ya Hyatt Regency, Posta jijini Dar kulipokuwa na hafla ya kuzindua taasisi ya kusaidia watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja na bidhaa ya manukato ya De La Boss iliyoandaliwa na Ofisa Habari wa Klabu ya Simba, Haji Manara.

download latest music    

Katikati ya hafla hiyo, Steve aliyekuwa ameongozana na JB alijigamba mbele ya watu kuwa kwa sasa analindwa naye jambo liliolofanya wengi kuangua vicheko.

Nina bodigadi huyu hapa (JB) na mimi nimekuwa mmojawapo kati ya wanaolindwa”.

Katika kuonyesha tukio hilo lilikuwa la utani Steve alionekana kumtaka JB amsogezee gari lake ili kumuiga Diamond ambaye alionekana na mabodyguard wawili na walionekana kumfungulia milango ya gari, JB aligoma na kila mmoja kuondoka kivyake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.