Steve Nyerere Anena Haya Baada Ya Lulu Kuachiwa Huru

Muigizaji wa Bongo movie na Mwanaharakati wa siasa Steve Nyerere amefunguka baada ya Muigizaji mwenzake Elizabeth Michael kuachiwa huru mapema jana.

Siku ya jana Jeshi la Magereza lilitangaza rasmi kupitia barua yao walioiachia Kwenye vyombo vya habari kuwa Elizabeth Michael ameachiwa huru rasmi na kwenda kutumikia kifungo cha nje.

download latest music    

Baada ya Lulu kuachiwa rasmi Steve Nyerere ambaye pia ni kiongozi Kwenye tasnia ya Bongo movie amemualika rasmi Lulu katika harakati za kuijenga upya tasnia hiyo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Steve Nyerere aliandika ujumbe huu:

LULU NI.JAMBO LA.KUSHUKURU SANA KWANI KILA PITO NAAMINI MUNGU YUPO.PAMOJA NAWE,NICHUKUE NAFASI HII KWA DHATI KABISA KUMSHUKURU MH RAIS JOHN POMBE MAGUFURI KWA MSAMAHA HUUU NAAMINI UMEFANYA JAMBO JEMA SANA RAIS WANGU,NIIPONGEZE MAHAKAMA PIA NA WADAU WOTE MLIO KUWA MNAMUOMBEA MWENZETU KUTOKA ,FAMILY, NJOO LULU TEJENGE TASNIA YETU SASA“.

Mara baada ya taarifa kusambaa kuwa Lilu ameachiwa huru wasanii wenzake wengi walionesha kufurahishwa na kitendo hiko.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.