Steve Nyerere asema asihusishwe na scandal ya audio ya Wema Sepetu

Rafiki wa karibu wa Wema Sepetu amefunguka kudai kuwa hataki watanzania wamuhusishe na audio ambayo Mrembo huyo anasikika akiongea na Mbowe.

Steve Nyerere ambaye ni mchekeshaji anayejulikana sana Afrika Mashariki alitaka Watanzania wajue kwamba hawezi kumfanyia rafiki wake wa karibu jambo kama hilo alipokuwa akizungumza na Bongo 5. Steve alisema,

download latest music    

“Sio mimi yule na siwezi kufanya kitu kama kile, Ile sauti ukiisikiliza kwa makini utajua sio mimi na siwezi kufanya hivyo,”

Mbowe hata hivyo amekana kuwa sauti hiyo sio yake lakini kwa sasa watalaamu wanafanya uchunguzi kujua nani aliyesambaza audio hiyo.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua