Sugu,Hata Nikisikia Amekufa Sitaenda-Faiza Ally.
Mwanadada asiyeishiwa na drama katika mitandao ya kijamii kila siku Faiza Ally amefunguka na kusema kuwa wala hajaumia kabisa baada ya Sugu kufungwa kwa sababu wao ni maadui hivyo hata haimshtui kumuona Sugu akiwa katika matatizo.
Faiza ambae alibahatika kupata mtoto mmoja wa kike kipindi alipokuwa katika mahusiano na Sugu , mtoto ambae anaishi naeo yeye mwenyewe kwa mara nyingi wamekuwa wakiingia katika migogoro na sugu kwa madai kuwa baba huyo hataki kutoa matumiz ya mtoto wake huyo.
hata hivyo hivi karibuni Sugu ambae ni msnaii lakini pia ni mwanasiasa na mbunge wa Mbeya ,Mjini alihukumiwa kifumgo cha miezi sita baabda ya kukutwa na hatia ya kutoa maneno ya uchochezi na ya kumkebei raisi.
Akiongea wikiend hii alipokuwa katika usiku wa Vikings Night, Faiza amesema kuwa amekisikia kifunmgo hicho lakini kwake hakijamuumiza kabisa na hata ikitokea siku Sugu akifa wala hataenda katika msiba wake.
sugu kuhukumiwa wala sijahumia wala ku-fell kitu chochote, ni maadui hata nisikie amekufa sitaenda.
Siku moja baada ya hukumu hiyo, faiza aliandika katika ukurasa wake wa instagram kuwa kinachomuumiza yeye kuhusu matukio ya sugu ni baada ya mtoto wake kwenda dukani na aliporudi alimwambia amemuona baba yake amepanda karandinga lakini kwa upande wake wala haumii na chochote kinachompa mzazi mwenzie huyo.