Msanii Kutoka Kenya Atangaza Kufa Kuoza Kwa Idris Sultan

Msanii wa muziki kutoka DRC Congo ambaye anafanya Shughuli zake za kimuziki nchini Kenya Alicious Theluji ametangaza kuwa amekufa ameoza kwa Mchekeshaji MBongo Idris Sultan.

Alicious ambaye amedai ameshindwa kujizua na hisia zake amefunguka na kudai kuwa kwa sasa hakuna mwanaume anayemvutia na kumpenda kama ilivyo kwa Idris Sultan.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha redio cha Citizen Kupitia kipindi cha Mseto East Africa, Alicious ameweka wazi kuwa Idris ni Crush Wake Lakini pia ni mtu ambaye anampenda sana.

Kwa sasa nipo Single, Idris Hivi karibuni nakuja Tanzania nina Media tour naomba unipokee Airport”.

Lakini pia mrembo huyo aliweka wazi vigezo vya nwanaume anayemtaka na kumtaja kabisa kuwa anamtaka Idris:

Navutiwa sana nadata, umeshawahi kuona mabega ya Idris wewe?”.

 

Sitaki Kusikia Kuhusu Ali Kiba na Diamond Wapeni Nafasi Wasanii Wengine- Alicious

Mwanamuziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo anayefanya kazi zake nchini Kenya amefunguka kuwa amechoshwa kusikia tu muziki wa Ali Kiba na Diamond bali amedai anataka kusikia wasnii wengine wengi wenye vipaji kutoka Tanzania.

Kwenye muziki wa Bongo fleva huwezi kukamiika bila ya kuwataja wasanii hawa wawili ambao ni Ali Kiba na Diamond ambao kutokana na ushindani uliopo baina yao umeweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa kukuza mziki wao lakini pia ushindani uliopo baina ya mashabiki zao umeweza kwa kiasi kikubwa kukuza miziki  yao na kuwafikisha hapa walipo leo, lakini kuna wasanii wengi ambao wanakosa nafasi kama walizonazo wasanii hao wawili.

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na Bongo 5, Alicious alifunguka kuwa amechoka kuulizwa maswali ya nani mkali kati ya Alikiba na Diamond bali anataka kusikiliza wanamuziki wengine kutoka Tanzania ambao nao wana vipaji;

Nakumbuka mara ya kwanza kuja Tanzania nilifanya interview nyingi na kila interview naulizwa unampenda Alikiba au Diamond? kila siku hadi ikafika wakati nikasema sitaki tena kusikia Ali Kiba na Diamond maana kuna wasanii wengine wengi Tanzania ambao wanafanya kazi vizuri. Lakini kusema kweli Diamond is very talented na Alikiba is very talented sioni maana ya kuwafanya wawe one against the other mi naona wote ni wasanii wakubwa wanajtahidikufanya muziki mzuri lakini nina uhakika kuna wasanii wengine Tanzania”.

Ushindani kati ya Ali Kiba na Diamond ni mzuri maana unamsaidia kila mmoja kukuza mziki wake na kufanya vizuri kutokana na changamoto wanayopeana lakini kwa upande mwingine nahisi umefika wakati wasanii wakubwa kama NavyKenzo, JohMakini, Ommy Dimpoz, Vanessa Mdee, Lady JD na wengineo wapewe nafasi ya kusikika zaidi kwani ninaweza nikasema wakati wasanii hao wawili wakubwa wakipaa kuna wasanii wengine wakubwa wanakosa sapoti ya kutosha.