Barnaba amjibu aliyekuwa mke wake kupitia ujumbe huu wa Instagram?

Barnaba na aliyekuwa mke wake wameonekana kupashana kupitia mitndao yao ya Instagram. Hii ni baada ya mrembo huyo aliyekuwa mke wake ambaye pia ni mzazi mwenziye, kuposti picha akiwa na mpenzi wake wa sasa mitandaoni huku akiandika ujumbe unaoelezea sababu za ndoa yao kuvunjika.

Hata hivyo Barnaba naye aliandika ujumbe kwenye ukurasa wake wa Instagram huku akiwasifia wanawake – lakini mashabiki wake wanaonelea kuwa alikuwa anamjibu mke wake.

Alindika kusema;

“Mama aliniambia ukimtukana mwanamke basi umenitukana na mimi, siku zote nawaona kama mama zangu, hongera wanawake wote duniani, salamu zangu juu yenu Jumapili ya leo nawapenda sana, na wale mliopoteza mama zenu fanyeni ibada juu yao waweze punguziwa adhabu ya kifo au kufutiwa kabisa, Bwana Yesu asifiwe sana Jumapili ya Mungu tumpe Mungu Wakristo wenzangu”

Hii ndio sababu Barnaba hataki kufanishwa na mtu yeyote

Msanii wa Bongo Fleva, Barnaba amesema kuwa hakuna msanii yeyote Bongo anayeweza kufananishwa naye kwa sababu yeye anauelewa muziki ambao anaoufanya.

Akizungumza na Mikito Nusunusu , Barnaba alisema kuwa kipaji chake amekitoa kwa mungu na anamshukuru Mungu kwa kumjalia kipaji cha kipekee kwenye muziki na kwamba ataendelea kukitendea haki. Alisema;

“Mimi ni mwanamuziki na si msanii, lazima kwanza utofautishe mambo hayo mawili, ndiyo maana ninaweza kutunga na kuimba na hata kutumia vyombo vyote vya muziki, hiyo ndiyo maana halisi ya mwanamuziki. Naomba sana nisifananishwe na mtu kwenye eneo hilo. Nilizaliwa kuburudisha watu na ninafanya muziki kama sehemu ya maisha yangu, siangalii fedha na masilahi, muziki uko kwenye damu,”