Darassa aeleza sababu za ‘Hasara Roho’ kutofanya vizuri kama ‘Muziki’

Muimbaji Darassa hivi karibuni aliachilia wimbo wake mpya ‘Hasara Roho’ lakini inaonekana kuwa mashabiki wake hawajaupokea kama wengi waliovyotarajia.

Ingawa wimbo huu hauna tofauti kubwa na Muziki sio wengi wameonyesha kuupenda na pia haujapata mtamzamo mkubwa kupitia YouTube.

Hata hivyo akizungumza kupitia kipindi cha 255 XXL cha Clouds FM, Darassa alisema kuwa mashabiki wake wamezoea Muziki zaidi kwa kuwa alikawia kuwachilia project mpya.

“Kitu ambacho kinatokea ni wimbo wa muziki umewakaa sana na kuusikiliza sana kwa namna moja au nyingine.”

Aliendelea kusema kosa lao ni kumtegemea kuachia wimbo kama Muziki ambacho hangeweza kufanya kwani kila anapoachia nyimbo lazima iwe tofauti.

“Mimi mwenyewe nilikaa sana na huu wimbo na kuupima, nikaona kuwa ni project ambayo inafaa kufuata na ikawatosha. Kwa hiyo kwa watu kukaa na kutegemea kuwa uje wimbo kama “Muziki” hiko ndio kitu kinachorudisha sanaa yetu nyuma.”

Baada ya ‘Muziki’ Darassa apanga kuachia nyimbo mpya

Darassa ambaye anatambulika Afrika Mashariki amewahaidi mashabiki wake nyimbo mpya ambayo aitawachilia hivi karibuni. Nyimbo hii inakuja miezi mitano baada ya kuachia Muziki ambayo imefanya vizuri baada ya kuangaliwa mara 7,056,225 YouTube.

Nyimbo hii ambayo inaitwa Hasara Roho ndio itakuwa project yake ya kwanza mwaka huu na mashabiki wake wameonyesha furaha kwani wameigonja project nyingine kutoka kwa Darassa.

Darassa

Kupitia Instagram yake Darassa aliandika kusema,

“Good morning from Bongo Tanzania East Africa to the Top of the world!. Nataka kusema asanteni sana kwa love na support ambayo mmetupatia kwenye project yetu ya ‘Muziki’ na kuipelekea kuwa National Anthem. Hakuna neno linaweza kumaanisha thamani yenu kwetu! God bless you all usikose kusikiliza project yetu mpya leo ??? #CMG#HasarARoho,”

Hanscana ambaye ni mmoja wa manager wake aliambia Bongo5,

“Sisi tumejiandaa vizuri kwa sababu tunajua mashabiki wanataka nini. Maandalizi ni makubwa sana, yaani ni kama tunaandaa Marais 5 wa nchi. Kwahiyo tumejipanga vizuri kuhakikisha jamaa anarudi vizuri katika game,”