Esma :Wema Bado Ana Umuhimu Sana Kwangu

Mwandada anaejihusisha na mitindo kwa sasa ambae ni dada yake na msanii mkubwa nchini, Esma Platinumz amefunguka na kusema kuwa pamoja na kwamba mwanadada Wema Sepetu ameshaachana na kaka yake Diamond Platinumz yeye hawezi kuachana urafiki na Wema kwa sababu hiyo kwa kuwa bado ana umuhimu sana kwake.

Esma amesema hayo baada ya siku za hivi karibuni msanii huyo kuonekana kuwa karibu sana na familia ya diamond platinumz hata siku ya birthday ya Esma, Wema Sepetu alimtakia kheri ya kuzaliwa mwanadada huyo katika ukurasa wake wa instagram.

Akiongea na waandishi wa habari, Esma amesema kuwa hawezi kuwa anakosana na kila mwanamke anaeachana na kaka yake na kupatana na wale alionao katika mahusiano kwa sababu hata yeye ni mtu mzima anahitaji kuwa na marafiki hivyo hawezi kugombana na Wema.

jamani hata kidogo Wema siwezi kumuweka pembeni,hata kama aliachana na kaka yangu  lakini kwangu ana umuhimu sana.kama kila anaeachana na kaka na mimi inabidi niwe nae mbali basi inabidi nikifa nikazikwe Uganda au Afrika Kusini.

Wema na Diamond walikuwa katika mapenzi kwa muda mrefu na baadae kuachana lakini esma hakuwahi kugombana mwanadada huyo,hata hivyo kipindi cha hivi karibuni kumekuwa na sekeseke linalowafanya familia ya Diamond kutofautiana na Zari the bossy ambae ni mzazi mwenzie na Diamond.

Hata hivyo huko nyuma zilishawahi kutokea tetesi kuwa kuna utofauti mkubwa wa kimahusiano kati ya Esma Platinimz na wifi yake Zari , kitu kinachomfanya hata esma kushindwa kuhudhuria sherehe nyingi ambazo kaka yake anakuwa anazifanya zilizokuwa zikimshirikisha Zari, lakini hivi karibuni esma alionekana katika sherehe ya wcb ambayo zari hakuwepo na Wema Sepetu alikuwa amearikwa.

 

Esma Afunguka Sababu ya Kutohudhulia Party ya Zari S.A

Kumekuwa na maswali mengi watu wakijiuliza kuwa kwanini katika party kubwa ya familia ambayo Diamond aliifanya yeye na familia yake huko nchini Afrika ya Kusini dada yake Esma hakuwepo katka party hiyo na holidays zote ambazo familia hiyo ilisherekea nchini humo.

Ingawa kumekuwa na taarifa za chini chini kuwa hakuna maelewano mazuri kati ya Esma Platinumz na mwanamke aliyezaa na kaka yake huyo ( Zari ) kwa kipindi kirefu tangu kipindi ambacho Hamisa Mobeto  (mwanamke mwingine wa Diamond) alipojifungua ambapo dada wa msanii huyo alikuwa akionekana yupo karibu sana na Hamisa na kumuhudumia kwa kila kitu na kumfanya Zari kuchukia kitendo hicho na ndio maana wawili hao mpaka sasa hivi na kwamba Esma hajataka kwenda kwa sababu wamekuwa hawako vizuri kimahusiano.

Hata hivyo baada ya maneno hayo kusambaa sana ,kampuni ya habari ya GPL, iliamua kumtafuta Esma Platnumz na kumuuliza juu ya habri hizo ambazo zinasemekana kuwa zilisemwa na mtu wa karibu kabisa wa familia yao kuhusu kutoelewana kwake na wifi yake Zari na sababu ya yeye kutokuhudhuria katika party ya siku ya kuzaliwa na mtoto wa kaka yake ni kutokuelewana kwake na Zari.

Nisingeweza kuiacha biashara yangu na duka langu ambalo ni elifungua tu hivi karibuni eti niende kwenye pati,wateja wangu wasingenielewa kabisa  na ningerudi ingechukua muda mrefu kidogo kuwarejesha kwakweli.Watu wanapenda kuongea sana lakin ukweli ni kwamba mimi na Zari  hatuna tatizo lolote , kama hauamini siku nyingine akiandaa pati ntaenda tu. Alifunguka Esma Platinumz

Hata hivyo siku ya mkesha wa mwaka mpya Zari alipost video akiwa na wifi yake huyo na kusema kuwa wanavuka mwaka mpya kwa pamoja huku wakionekana na furaha.