Hii ndo sababu Diamond alirejea Tanzania kwa upesi baada ya kuzika mamake Zari

Diamond alisafiri kuelekea Uganda kwasababu ya mazishi ya mama mkwe wake ambaye aliaga dunia Alhamisi wiki jana akipata matibabu hospitalini.

Mamake Zari – Halima Hassan alizikwa Ijumaa kulingana na itikadi za Kieslamu ambayo inasema wafu wanafaa kuzikwa chini ya masaa 24 baada ya kifo.

Mama mkwe wa Diamond alizikwa Kalama, mji ambao uko katikati ya Uganda. Baba Tiffah alihudhuria mazisho hio huko Kalama.

Diamond akiwa kwa mazishi ya mama mkwe wake

Staa huyo hata hivyo aliabiri ndege kurudi Tanzania siku hio hio ya Ijumaa baada ya mwenda zake kuzikwa. Diamond alirejea Tanzania kwa upesi kwasababu alikua na show Jumamosi pale Leader Club.

“Mitihani ni sehem ya Maisha na Huletwa na Mwenyez Mungu , na Siku zote huletwa kwa sababu, na ndiomaana tumefunzwa kushukuru kwa kila jambo….. Allah nakushkuru kwa yote, Nakushkuru kwa kunifikisha Uganda na Kumaliza kila jambo salama….Naomba pia Uniongoze katika safari yangu hii ya sasa ya Kuelekea Dar es Salaam….na unitie nguvu siku ya kesho nikiwa kazini pale Leader Club… ? @mama_dangote,” Diamond aliandika.

Diamond na mamake wakiwa wanarejea Tanzania

 

Diamond na mamake walivyowasili Uganda kwasababu ya mazishi ya mamake Zari (Video)

Diamond Platnumz tayari amewasili nchini Uganda kumfariji mkewe Zari Hassan ambaye alimpoteza mamake mzazi Alhamisi asubuhi.

Mamake Zari – Halima Hassan aliaga dunia akiwa anapata matibabu katika Nakasero Hospital jijini Kampala. Mwendazake alifariki kutokana na maradhi ya moyo.

Staa huyu wa wasafi alisafiri Uganda na mamake Sanura Sandra Kassim na meneja wake Babu Tale. Tazama video hapo chini uone jinsi Diamond aliwasili Uganda.