Idris Sultan Adaiwa Kumchukua Ex wa Diamond

Msanii wa Bongo movie na comedian maarufu Idris Sultan anadaiwa kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na Ex girlfriend wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Kumekuwa na tetesi kuwa Video vixen ambaye hakauki vituko Kwenye mitandao ya kijamii Irene Geofrey maarufu kama Lynn ana banjuka na Idris Sultan.

Tetesi za Mahusiano ya wawili hao zilianza juzikati ambapo watu wengi walipigia mstari baada ya mwanadada huyo kuposti picha ya Idris huku akiandika maneno ya kimahaba yalisomeka; “Babyboo baby boo bae.”

Baada ya Tetesi hizo kupamba moto Kwenye mitandao ya kijamii gazeti la Risasi Vibes, lilimsaka Lynn ambaye mara moja alikana kuwapo kwa Mahusiano hayo:

Unajua muda mwingine unaweza kuposti kitu halafu maneno yakajiandika yenyewe, sasa ndicho kilichonitokea na mimi sikutaka kufuta kwa sababu watu wangesema ni kiki.

Lakini Idris ni mshikaji wangu wa karibu sana na ninampenda anavyochekesha, watu wasinitengenezee mambo ambayo hayapo jamani“.

 

Baada Ya Diamond, Lynn Haamisha Majeshi Yake Kwa Chris Brown

Video vixen maarufu kabisa Irene Hillary maarufu kama Lynn aliyejizolea umaarufu Kupitia video ya Rayvanny ya wimbo wa ‘Kwetu’ amefunguka kuhusu mahaba mazito kwa supastaa wa kimataifa

Lynn alipata umaarufu baada ya kudaiwa kutoka kimapenzi na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz hadi kubeba mimba yake.

Lakini hivi sasa Lynn ameweka wazi kuwa mapenzi yake yote yanehamia kwa staa wa Muziki kutoka Marekani Chris Brown na kusema Staa Huyo anamkosesha usingizi akimuwaza.

Kwenye mahojiano na Risasi Jumamosi, Lynn alisema kuwa ametokea kumpenda sana mwanamuziki huyo kiasi ambacho haelewi atafanyaje ila anaomba katika maisha yake siku moja akutane naye, amueleze hisia zake.

“Hivi ulishawahi kumpenda mtu mpaka ukawa huelewi sababu? Sasa ndio mimi nilivyo kwa Chris, naamini siku nitaonana naye na kama ikitokea hivyo kwa kweli nitamfikishia hisia zangu, kama atakubali au kukataa, niwe tu nimemuambia, naamini nitakuwa na amani”.

Lynn ameonekana akimweka Chris Brown Kwenye ukurasa wake wa Instagram mara kwa mara na kutoa yake ya moyoni kwa Staa huyo.

Irene: Sina Mpango wa Kuolewa na Mwanaume Wa Bongo Ni Wababaishaji

Video vixen anayejulikana sana mitandaoni Irene Hillary maarufu kama Official Lynn amefunguka na kuweka wazi kuwa hana mpango wa Kuolewa na wanaume wa kibongo kwa sababu wengi wao ni wababaishaji.

Irene alijizolea umaarufu siku za nyuma kutokana na kuonekana katika video ya kwetu iliyoimbwa na Rayvanny Lakini pia umaarufu ulizidi baada ya kusemekana kutoka kimapenzi na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Risasi Jumamosi, Irene  alisema kuwa ameona wanaume wengi wa Kibongo wanapenda sana kuchezea wanawake hivyo haoni sababu ya kuutesa moyo wake kwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mbongo.

Yaani kwa niliyoyapitia sitarajii kabisa kuolewa na Mbongo wala sina wazo hilo kabisa maana naona wazi nitautesa moyo wangu bure“.