Lynn Adaiwa Kutimuliwa Kwenye Mjengo Aliokuwa Anaishi

Video vixen na msanii wa Bongo fleva Irene Louis maarifu kama Official Lynn amejikuta katika wakati mgumu baada ya taarifa kuenea kwenye Mitandao ya kijamii kuwa ametimuliwa kwenye mjengo aliokuwa anajiachia nao.

Miezi michache iliyopita Lynn ambaye amewahi kuwa kwenye mahusiano na Diamond Platnumz alizua gumzo Baada ya kuanika Mali zake kwenye Mitandao ya kijamii ikiwemo mjumba wa kifahari ambao alidai ni Mali yake.

Lakini mambo yamesemekana kumuendea kombo mrembo huyo kwani mjengo huo umeonekana kwenye page ya Dalali na kwa Jinsi inavyoonekana Nyumba ile ilikuwa ya kupangisha tu.

Dalali huyo ameweka wazi kuwa mjengo huo utakuwa wazi kuanzia mwezi wa tatu Baada ya mtu anayeishi hapo Hivi sasa (ambaye ni Lynn) kutegemewa kuhama.

Habari za kimbea mtandaoni zinasema kuwa mrembo huyo amemwagana pedeshee ambalo lilikuwa linasimamia shoo na hivyo kusababisha Kufulia.

Lynn ambaye Hivi sasa anafanya muziki wa Bongo fleva na anafanya vizuri na ngoma yake ya ‘Chafu’ hajasema chochote kuhusu sakata hilo Mpaka Hivi sasa.

 

Lynn Aweka Mitandao Ya Kijamii Kando Ili Kufanya Mambo Ya Msingi

Video vixen maarufu aliyegeukia muziki wa  Bongo fleva hivi karibuni Irene Charles maarufu kama Lynn amefunguka na kusema kuwa hivi sasa ameamua kuachana na Mitandao ya kijamii.

Lynn ambaye alikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz na kusababisha kukamata headlines kila siku Mitandaoni Lakini tangu mahusiano hayo yaishe Lynn amekuwa kimya sana.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Lynn alisema watu wengi sasa wamegundua kuwa maisha ya mitandaoni yanadanganya na kama mtu asipokuwa makini, hawezi kufanya chochote cha maana zaidi ya kudili na mitandao ya kijamii.

Nilikaa na kuwaza kuhusiana na maisha ya mtandaoni maana yanaweza kukufanya ukawa bize bila sababu ya msingi hivyo hata ukiniona kwenye mitandao ni kwa sababu maalum tu“.

 

Lynn Akiri Kuwahi Kuwa na Tabia Ya Udokozi

Video vixen maarufu ambaye sasa ni Msanii wa Bongo fleva Irene Godfrey Louis maarufu kama Lynn amefunguka na kuweka wazi kuwa aliwahi kuwa na tabia ya udokozi.

Mrembo huyo ambaye amewahi kuwa Mpenzi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, ametoa siri  jinsi alivyokuwa anapen­da kula maziwa ya unga kiasi kwamba alikuwa anadiriki kudokoa pesa za mama yake ili mradi tu akanunue maziwa hayo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la  Ijumaa Wikienda, Lynn al­isema alipokuwa mdogo alikuwa anapenda sana kulamba maziwa ya unga, ikawa asipoyapata ana­kosa amani hivyo alifanya kila awezalo apate pesa akayanunue.

“Yaani nilikuwa napen­da sana kulamba maziwa ya unga kiasi kwamba nilianza kuwa na katabia ka’ kudokoa pesa za mama ilimradi tu ni­pate maziwa ila ikafika wakati mama ikambidi azoee hiyo hali, akawa ananipa pesa nika­nunue ili nisizoee tabia ya wizi”.

Lynn Alipay’s umaarufu Baada ya kuwa video queen kwenye wimbo wa Rayvanny ‘Kwetu’ na Hivi karibuni ametoa wimbo wa kwanza na kutangaza rasmi kuingia kwenye muziki.

 

“Naanzaje Labda Kutembea na Shetta”- Lynn

Videi vixen ambaye Hivi karibuni aligeukia gani ya  Bongo fleva, Irene Godfrey maarufu kama Official Lynn amefunguka na kudai hawezi hata siku moja kutembea na msanii mwenzake Nurdin Bilal ‘Shetta.

Lynn amesemameweka hayo Baada ya tetesi zilizowahi kusambaaa kwenye Mitandao ya kijamii kuwa wawili hao ni wapenzi kutokana na ukaribu ambao wamekuwa nao sasa.

Katika mahojiano yake na Gazeti la  Risasi Jumamosi, Lyyn alisema kuwa ukaribu wake na Shetta unatokana na kazi wanayoifanya kwa pamoja lakini alishangazwa na maneno kwamba wanatoka kimapenzi kitu ambacho siyo kweli.

Hivi naanzaje kutoka na Shetta jamani kwa hiyo kila mtu nitakayekuwa naye karibu ni bwana wangu? Shetta ni mshikaji wangu, siwezi kutoka naye na huku Afrika Kusini tumekuja kikazi wala siyo kula bata kama watu wanavyosema ila kwa kuwa wanapenda kutunga uongo waendelee tu kuamini, sina muda wa kuwalazimisha waelewe, napiga kazi tu”.

 

Kim Nana Afungukia Tetesi Za Bifu na Lynn

Video vixen maarufu kama Lilian Kessy ‘Kimnana’ amefunguka na kudai kuwa yeye na video queen mwenzake Irene Louis ‘Lynn’ hawana Bifu kama inavyodaiwa.

Tetesi za kuwepo kwa Bifu kati ya warembo hao zilizuka Baada ya warembo hao wawili wote kudaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Kim Nana amefunguka  kuwa watu wamekuwa wakizungumza mengi kuwa ana bifu na Lynn, lakini hawajawahi kuwa maadui hata siku moja na Lynn ni kama mdogo wake na hata wakikutana wanasalimiana vizuri na kuzungumza.

Lynn ni mshkaji wangu, hatuna bifu kabisa ndiyo maana hata hivi karibuni niliposti kipande cha video nikiwa naimba wimbo wake wa Chafu kwa lengo la kumsapoti hivyo wanaosema tuna bifu imekula kwao maana siyo kweli”.

 

“Diamond Ruksa Amuoe Tanasha”- Lynn

Video vixen na msanii wa muziki wa Bongo fleva Irene Godfrey Louis amefunguka na kumpa baraka zote aliyekuwa mpenzi wake Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz  kumuoa Mpenzi wake mpya Tanasha Donna Oketh.

Kwenye mahojiano aliyofanya na  Global PublishersLynn ambaye aliwahi kutajwa kuwa mbioni kuolewa na Diamond alisema anawashangaa wanaosema anaumia juu ya kitendo cha Diamond kutangaza kumuoa Tanasha, jambo ambalo si kweli.

Sina kinyongo, Diamond amuoe Tanasha hata kesho maana ni jambo la heri. Ninafurahi sana kwa sababu Diamond ni mshkaji wangu sana na si vinginevyo”.

Diamond aliweka wazi mahusiano yake na mrembo Tanasha kutoka Kenya na kutangaza ndoa yao mara moja hali iliyopelekea taarifa kusambaa kuwa Lynn amemwaga na msanii huyo aliyekuwa kwenye mahusiano naye.

Lynn Akiri Kuvutiwa na Rayvanny na Dogo Janja

Video vixen na msanii wa Bongo fleva Irene Godfrey Louis maarufu kama Lynn ameibuka na kuweka wazi kuwa wasanii waliomvutia kwenye Sanaa ni Mastaa wa Bongo fleva Rayvanny na Dogo Janja.

Wiki mbili ziizopita Lynn aliingia rasmi kwenye tasnia ya Bongo Fleva kwa kutambulisha wimbo Wake Mpya ‘Chafu’.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Jumamosi, Lynn alisema kwa kipindi kirefu alikuwa na nia ila alikosa mtu wa kumshauri, lakini baada ya kuwasikilizisha nyimbo zake, Rayvanny na Dogo Janja walimtia moyo kuwa anaweza.

Muziki ni moja ya malengo yaliyokuwa ndani yangu, lakini ndoto zangu niliona kama zinakufa kutokana na baadhi ya watu kunikatisha tamaa. Lakini ilikuwa tofauti kwa Rayvanny na Dogo Janja ambao walinipa moyo kuwa naweza ndipo nikatoa wimbo wangu haraka”.

Lyyn ambaye ameachia ngoma inayokwenda kwa jina la Chafu na kusifia mapokezi kuwa ni mazuri kuliko alivyotegemea hivyo amepanga kuachia mwingine fasta.

 

 

Lynn Afungukia Mapenzi Yake Kwa Jacqueline Wolper

Video Vixen na msanii wa Bongo fleva Irene Louis maarufu kama Lynn amefunguka na kuweka wazi kuwa anamkubali sana mwanadada mkali wa fasheni Jacqueline Wolper.

Lynn alifunguka hayo Baada ya kuulizwa sababu iliyomfanya Mpaka awe namfuatilia Msanii mmoja tu Bongo kupitia ukurasa wake wa Instagram na sio wasanii wengine.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha habari nchini, Lynn ameweka wazi kuwa sababu ya kwanza ni kuwa anamkubali sana Wolper na pili ndio mtu ambaye kibongo bongo anaendana naye:

Mimi naona toka tujuane tunakuwa tupo sawa tu kishikaji tunaongea, kwa hiyo yeye kama kuna kitu tumefanana ndio maana tumekuwa hivyo. Nahisi damu zetu zimeendana, labda wengine watakuja”.

Siku chache zilizopita  Jacqueline Wolper alifabya bonge la party kwa ajili ya kusherehekea miaka kadhaa ya kuzaliwa kwake, Mwanadada huyo ( Lynn) ni miongoni watu waliojumuika.

Lynn Akiri Kutamani Ndoa Katika Umri Wa Miaka 19

Muuza nyago maarufu katika video za wasanii mbali mbali Irene Godfrey maarufu kwenye social media Kama Official Lynn amefunguka na kudai anatamani sana ndoa hata Kama ana umri wa miaka kumi na Tisa tu.

Kwenye interview yake na Gazeti la Ijumaa, Lyyn aliyewahi kudaiwa kutoka kimapenzi na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ alisema kwamba japokuwa ndoa ni mipango ya Mungu lakini yeye anatamani sana kuolewa na kutulia katika ndoa yake kwa sababu itamuepusha na mengi ambayo anazushiwa sasa.

Unajua zamani malengo yangu yalikuwa kuolewa nikiwa na umri wa miaka 26 lakini kila siku zinavyozidi kwenda ndio nazidi kutamani ndoa kwa kweli sijui kwa sababu mtu wangu ananijali sana na kunipa mapenzi ya kweli, ingawa sitakuja kuweka mahusiano yangu wazi kwa sababu bebi wangu hapendi labda mtakuja kumjua tukioana“.

Lakini pia Lynn amejitapa kuwa Bongo yeye pekee ndiye staa ambaye anamiliki vitu Bongo vya thalami katika umri mdogo Kama vile Magari manne ya kifahari na Nyumba mbili.

Diamond Ruksa Kumuoa Kim Nana-Lynn

Video vixen aliyejizolea umaarufu Kupitia kichupa cha wimbo wa ‘Kwetu’ wa Msanii Rayvanny, Irene Hillary maarufu kama Lynn amefunguka na kusema ni ruksa kabisa Kwa Diamond kumuoa Kim Nana.

Lynn alifunguka hayo siku chache Baada ya warembo hao wawili wanaosemekana kufaidi Penzi la staa huyo wa Bongo fleva kugongana katika shoo ya Wasafi Festival mkoani Mtwara.

Gazeti la Risasi linaripoti kuwa warembo hao ni Kama paka na panya kutokana na wote kumpenda staa huyo hivyo walivyokutana Mkoani Mtwara kila mmoja alipooza na kuonekana wakiangaliana kwa jicho la uhasama.

Kama utakuwa uliwafuatilia walipopanda jukwaani utakuwa uliwashuhudia walivyokuwa wakikatana jicho la ukali.

Lakini Kim anaonekana kuibuka kidedea maana tofauti na Lynn, yeye alionekana mwenye furaha huku akikata nyonga kuashiria hakuwa na stresi kama mwenzake.

Hata wakati wa kurudi Dar, Lynn alipanda gari la wanenguaji na njiani alionekana kabisa hana furaha, tofauti na Kim aliyepanda kwenye gari moja na wanamuziki wa Wasafi na kujitwalia mapozi kama yote hivyo kumaliza kabisa umalkia wa Lynn ndani ya Wasafi”.

Baada ya tetesi hizo za kuwepo wivu wa kimapenzi Lynn alipiga stori na Gazeti hilo na kufunguka kuhusu  mahusiano yake na  Diamond na Kim Nana.

Unajua kuna kitu watu hawakijui kuhusu mimi na Diamond. Mimi na Diamond hatua uhusiano wowote ule.

Diamond ni mshkaji wangu sana kwa hiyo hata akimuoa Kim haiwezi kuniuma kwa sababu atakuwa wifi yangu na nimebariki amuoe tu wala sina tatizo lolote,

Povu la Shilole Kwa Media Zinazompa Kiki Lynn

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole ametoa Povu zito kwa media ambazo amedai zimekuwa zikitoa Kiki za bure kwa watu ambao hawana vipaji na sio wasanii.

Watu wengi wamekuwa wakihoji kuhusiana na mafanikio ya ghafla na umaarufu wa video vixen Irene Hillary maarufu kama Lynn huku wengi wakitaka kujua ni kazi gani hasa anazifanya na kumpatia pesa alizonazo pamoja na mali.

Shilole ameamua kufunguka kuhusiana na media zinazompa air time officiallynn na kuuliza wadau ni kitu gani hasa amekifanya kwenye jamii mpaka kinawafanya wampe nafasi sana.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Shilole alimwaga Povu hilo na kuandika:

Tuseme ukweli huyu dada anafanya kitu gani mpaka mwandishi aseme anatreand je anafanya movie ni mwanamuzik na amefanya nini ktk jamii ? Jamani waandishi wa habari kuweni makini ndio maana mnatuletea mambo ya akina Amber Rutty”.

Watakuja kuchafua sanaa yetu tuonekane wote wapumbavu kwa ajili ya mtu mmoja anapewa promo ya kijinga ili wapate habari Alafu wanaweka YouTube bila kujali mnazalilisha tasnia yetu wandishi wengine shame on you”.

Lynn alijizolea umaarufu Baada ya mahusiano na Diamond Platnumz ambapo miezi michache iliyopita Msanii huyo alimnunulia mrembo huyo gari kwenye birthday yake.

 

Ukaribu Wa Petit Man na Lynn Wazua Gumzo Ukumbini

Mdau mkubwa wa muziki wa Bongo fleva na ambaye pia ni meneja wa wasanii wengi Hamad Manungwa ‘Petit Man’ na mrembo Irene Hillary maarufu kama Lynn wamezua gumzo kutokana na ukaribu wao.

Global Publishers wanaripoti kuwa  wawili hao waluonekana pamoja ndani ya Klabu ya Next Door Arena iliyopo Masaki jijini Dar ambapo mwanamuziki, Faustina Charles ‘Nandy’ alikuwa akisheherekea kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa ‘bethidei’ samba mba na kuzindua albamu yake iitwayo African Princes.

Wawili hao wakiwa ukumbini hapo walionekana kuwa na kikao kizito na pozi lao kuzua mino ng’ono ndipo walipofuatwa na GPL, ili kujua walicho kuwa wakijadiliana ambapo Petit Man alisema wako kwenye mikakati ya kikazi.

Usione tuko kwenye pozi hili na tunano ng’onezana ni kwamba kuna kitu tunaandaa na Lynn na muda si mrefu tunataka kufanya bonge la sapraiz kwa mashabiki wa burudani hivyo watu wasitufikirie vibaya“.

Ukaribu wao ukimya gumzo kutokana na kwamba Petit alikuwa mume wa Esma Dada yake na Diamond na Lynn alikuwa Mpenzi wa Diamond Platnumz.

Nai Amtuhumu Lynn Kwa Kupenda Kudanga

Video vixen na mpenzi wa Rapa Moni Centrozone, Nai ameibuka na kumtuhumu Mrembo Irene maarufu kama Lynn kuwa mdangaji mkubwa hapa mjinI.

Lynn ameibuka na kudai kuwa yeye ni binti Mchapakazi na sio mtegemea kudanga kama ilivyokuwa kwa Lynn ambaye anaishi kwa kutegemea madanga.

Kwenye mahojiano aliyofanya na  Gazeti la  Risasi Vibes, Nai alimtaka Lynn kuacha kumzungumzia vibaya katika biashara zake ndogondogo anazozifanya kwa ajili ya kujipatia kipato na badala yake afanye mambo yake yanayomuhusu.

Nashangaa kwa nini huyo Lynn anadharau biashara yangu, kitu ambacho sikipendi anaona kazi zangu hazina maana kwa kuwa amezoea kudanga kwa wanaume ndiyo apate pesa, kwa hiyo naomba aache kudharau biashara yangu kwa sababu ndiyo inanifanya mimi niwe hapa”.

Hivi karibuni Lynn ameibua maswali mengi baada ya kuanika mali zake anazomiliki Ikiwa pamoja na nyumba tatu na magari manne ya kifahari na kupelekea watu kusema anadanga kwani hana kazi anayefanya inayoweza kumuingizia kipato kikubwa cha kumiliki mali zote hizo.

Lynn Awatolea Povu Watu Wanaohoji Utajiri Alionao

Video vixen maarufu katika tasnia ya Bongo fleva Irene Jeffrey Louis maarufu kama Lynn amefunguka na kuwatolea povu zito watu ambao wamekuwa wakihoji utajiri ambao amekuwa akijionyesha nao Kwenye mitandao ya kijamii.

 

Wiki iliyopita Lynn aliweka wazi kuwa pamoja na kuwa mdogo mwenye umri wa miaka 18 tu lakini mpaka hivi sasa anamiliki Magari manne ya kifahari na nyumba nne.

Baada ya Lynn kuonekana akipiga picha na magari hayo na hata kwenye nyumba hizo tetesi zilianza alidaiwa kwa kuazima magari na hata nyumba sio mali zake.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Lynn aliweka hati zake zote za magari ili Kudhihirisha kuwa yeye ndio mmiliki halali wa magari yake yote:

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Lynn amewatolea povu mashabiki ambao wamekuwa wakimtuhumu kwa kujionyesha na mali ambazo si zake

Ndiyo mali ni za kwangu. Mbona huwa ninaposti mitandaoni na hati zake kama hati za nyumba na magari yangu? Ninaponunua magari kwani huwa hamuoni? Tena hivyo ni baadhi tu maana nina nyumba nne na magari manne. Pia jumlisha na gari lingine nililonunuliwa Jumanne (wiki hii) na nimeposti kadi ya gari ikiwa na jina langu, sasa ni ukweli gani ambao watu wanataka kujua kutoka kwangu?.

Unajua kinachowauma watu ni kwa sababu ninamiliki vitu vingi vya thamani halafu ndiyo kwanza nina umri wa miaka kumi na nane, nimewapita hadi niliowakuta wakiwika mjini, kiukweli inauma na hata ningekuwa mimi ningeumia kama wanavyoumia, ila sidangi jamani nina ishu zangu kibao ninafanya hapa mjini halafu naona watu wananichukulia poa kama wanaona kudanga rahisi si wadange na wao (alicheka na kukata simu).”.

Husna Ajaribu Bahati Yake Kwa Diamond

Mrembo ambaye aliwahi kufanya vyema Kwenye Mashindano ya Miss Tanzania 2011/2012 Husna Maulid ameibuka na kudai kuwa na yeye ni mmoja kati ya warembo wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Sakata hilo la Husna lilitokea siku chache zilizopita baada ya kuweka picha yake Instagram na kusindikiza na maneno ‘Roho Ya Simba’ na kuonyesha yupo Madale nyumbani kwa Diamond jambo lililosababisha mashabiki kumjia juu.

Mashabiki walimshambulia kwa kitendo cha kumuweka na yeye kwa Diamond ilhali anajua kwamba tayari ana wanawake kadhaa tayari Kwenye Mahusiano naye.

Baada ya povu hilo la mashabiki, Husna alifanya mahojiano na Global Publishers ambapo alimwaga povu kwa watu wanaosema anamtaka Diamond ambaye ni bwana wa Lynn.

Unajua kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, huyo Lynn ni nani, siwezi kumuhofia yeye wala mwanamke mwingine yeyote maana kila mtu na bahati yake, wanaotukana watukane watachoka”.

Hivi Diamond tayari amekwisha mmwaga Lyyn na Yupo Kwenye Mahusiano na Mrembo mwingine anayeitwa KimNana.

Lynn Amkana Diamond Baada Ya Kumwagwa

Socialite na Video vixen maarufu Kwenye mitandao ya kijamii Irene Godfrey maarufu kama Lynn au Officiallyn ameibuka na kudai hajawahi kuwa kwenye  uhusiano wa Kimapenzi na Diamond.

Lynn alijipatia umaarufu baada ya kutokea kwenye video ya wimbo wa Rayvanny ‘Kwetu’ lakini baada ya hapo amekuwa maarufu kwa kusemekana kuwa Kwenye Mahusiano na Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Wiki chache zilizopita Lynn alitrend Kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuonekana mikononi mwa Diamond kama mpenzi wake kwa siku kadhaa na hata kudaiwa kumfanyia bonge la Birthday party na hata kumnunulia gari.

Lakini Penzi hilo halikuwa la muda mrefu kwani siku mbili baadae Diamond alionekana na warembo wengine wawili tofauti ikiwemo Tunda na Kimnana ambaye yupo naye mpaka leo.

Sasa Lynn anaibuka na kusema hajawahi kuwa Kwenye Mahusiano na Diamond na kudai ana mpenzi wake ambaye jana tu ametoka kumzawadia gari aina ya BMW.

Kwenye Interview yake na kituo kimoja cha habari Lynn amemwaga povu hili kuhusu Diamond:

Hakuna kitu sipendi kama watu wanao judge watu Kwenye social media na kuongea vitu ambavyo hawavijui kama wewe apo unaponiambia natoka na Diamond! Jamani mimi sipo na huyo mtu nina boyfriend wangu ambaye Nipo naye Kwenye relationship strong kabisa na muda wowote watu wanaweza kumjua”.

Siju za hivi karibuni Lynn alionekana katika vita ya maneno na wanawake kadhaa wa Diamond kama vile Hamisa, Kimnana na Tunda lakini bado anadai hamjui Diamond na hajawahi kuwa naye.