Uwoya aeleza sababu za muvi za bongo kupotea sokoni

Uwoya ambaye ni mmoja wa waigizaji maarufu Bongo hivi karibuni alifunguka kueleza sababu za soko la muvi za kibongo kwenda chini.

Uwoya
Uwoya

Akizungumza na Global Publisherz, muigizaji huyo alisema kuwa kuna changamoto kadhaa ambazo zimechangia huku akiwalaumu wasambazaji wa muvi za kibongo wanazoziuza muvi hizi kwa bei ya chini.

Tazama mahojiano yake na Global Publisherz hapa;

Swali: Labda mimi siyo mfuatiliaji sana, lakini naona kama filamu zimesimama hivi au?

Uwoya: Zimesimama unamaanisha nini? Yaani hazizalishwi tena au?

Swali: Ninamaanisha haziko kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma, filamu zilikuwa nyingi sokoni na watu wakizigombea, sasa hivi sizioni.

Uwoya: Ni kweli, sasa hivi wasanii wamepunguza kutengeneza kazi mpya, sababu kubwa ni soko, limekuwa gumu sana.

Swali: Limekuwa gumu kivipi?

Uwoya: Hapa pana changamoto nyingi, kwanza kwa wasambazaji wenyewe na pia kwa wanunuzi. Kwa upande wa usambazaji, wananunua kazi kwa bei ambayo inatuumiza na mara nyingi tunakuwa hatuna jinsi, ni bora tufanye kazi tuonekane kuliko kukaa tu nyumbani.

Swali: Huoni kuwa ubora duni wa kazi zenu ulichangia kwa wasambazaji kununua kwa bei ndogo?

Uwoya: Wakati mwingine uduni wa kazi unatokana na haohao wasambazaji ambao wana bei zao.

 

Mwigizaji wa filamu Batuli afunguka kuhusu beef yake na Irene Uwoya

Yobnesh Yusuph anayejulikana kwa umaarufu kama ‘Batuli’ amedai kuwa yeye hana beef yoyote na mwigizaji wa kibongo, Irene Uwoya. Mwigizaji huyo aliendelea kusema kuwa Uwoya ndiye anapaswa kueleza beef yao inatokana na nini kwani yeye ndiye anayesambaza maneno haya.

Batuli
Batuli

Batuli aliendelea kusema kuwa hana muda wa kuanzisha ugomvi na mtu yoyote haswa Uwoya. Kulingana na yeye amewazibia watu macho na maskio wanoeneza stori hizi mitandaoni. Batuli alisema,

“Sina muda wa kugombana na Uwoya, kama kuna tatizo aulizwe yeye siwezi kuusemea moyo wake.”

Uwoya
Uwoya

Uwoya alipotafutwa kupitia simu yake Mwigizaji huyu hakushika wala kujibu SMS kuhusu beef hii yake na Batuli. Kwani kuna nini?