“Siwezi kutoa nyimbo mpya kila siku”-Lady Jay Dee

Msanii  mkongwe kabisa wa kike kutoka tanzania ambae alianza muziki na bado  anaendelea nao kwa mud amrefu pamoja na kuwa game linazidi kubadilika lakini bado yuko imara katika kazi zake mwanadada jay dee  amefunguka na kusema kuwa hawezi kuwa anatoa nyimbo mpya  kila siku kwa sababu anaamini kuwa nyimbo zake ni nyimbo zenye hisia sana na huishi muda mrefu hivyo si lazima kutoa nyimbo nyingi kwa wakati mmoja.

Mwana dada huyo ambae hivi juzi ametoa wimbo mpya unaokwenda na jina la ‘i miss you’ ambao umetengenezwa na producer man water ambae pia ametengeneza nyimbo zake nyingine nyingi ikiwepo ule wa ndindindi  anasema kwa sasa wasanii wengi wamekuwa wakitoa nyimbo mfululizo  bila kujali kuwa wimbo uliopita umekaa kwa muda gani,”siwezi kuwa natoa nyimbo mpya kila siku ,kwa sababu nyimbo zangu ni za hisia sana ambazo zinaweza kukaa hata  miaka kumi.Ni bora nitoe wimbo mmoja  kwa mwaka  lakini uwe  unaishi miaka mingi kwa  ladha ile ile  siku zote‘  amesema jay dee

Akizungumza na kipindi cha planet bongo cha East Africa Radio ,pia lady jay dee amepata nafasi ya kuzungumziz kwa ufupi hali ya usalama inayoendelea nchi ikiwepo kuuawa na kutekwa kwa baadhi ya watu maarufu akiwepo msanii wenzio roma mkatoliki lady jay dee anasema “kitendo cha mtu kuweza kupigwa risasi  hadharani inatishia amani sana, vilevile kuna wasanii walikuwa wametekwa,unaogopa,sehemu yenye amani vitu kama hivi haviwezi kutokea,ninaweza nisiwe na maneno ya kusema nikabaki kusikitika tu kwasababu sio mambo mazuri haya yanayotokea,na yanaonyesha kuwa sio kuzuri tunakoelekea”  ameongezea dada mkubwa.

Lady jay dee ni moja  kati ya wasanii wakongwe kabisa wenye mchango mkubwa katika kukuza sekta ya muziki wa bongo fleva Tanzania na amekaa katika kazi hii zaidi ya miaka kumi na bado nyimbo zake zimekuwa ni nyimbo zenye kupendwa na mashabiki sana ,kiasi kwamba hata zile  za zamani bado zinapendwa na watu .

 

“Jaydee ana mapenzi ya kweli” Ray C afunguka kuhusu uhusiano wake na Lady Jay Dee

Ray C alizungumzia uhusiano wake na Lady Jaydee katika mahojiano aliyofanya hivi karibuni na Mwanaspoti. Mrembo huyo alimsifu Jaydee kwa kuwa na mapenzi ya kweli.

Ray C alisema kuwa Jaydee alimwonyesha upendo sana katika kipindi alipokuwa ameathirika na utumizi wa dawa za kulevya.

“Jaydee ana mapenzi ya kweli kwa msanii mwenzake. Hataki kuona anaanguka…ninampenda sana kwa moyo wake wa upendo,” Ray C alisema.

Mrembo huyo pia ushauri wake kwa matumizi ya dawa za kulevya, alisema kuwa serikali inafaa ijitahidi kutoa elimu mashuleni kuhusu athari za kutumia dawa za kulevya.

“Mie naiomba tu Serikali ijitahidi kutoa elimu mashuleni kuhusu athari za kutumia dawa za kulevya, kwani wengi wanaoathirika kwa sasa ni vijana tena wadogo na wengine ni wanafunzi na hao wanafunzi hutumia muda wa mapumziko kutumia dawa hizo hivyo kupewa elimu ni muhimu kwani hawajui athari zake wanajiingiza kama mimi nilivyojiingizaga bila kujua,” anasema.

 

Rama D afunguka kuhusu uhusiano wake na Lady Jaydee

Mwimbaji wa R&B Rama D ameweka kikomo kwa uvumi unaoendelea kwenye mitandao ya kijamii kuwa yeye na Lady Jaydee ni wapenzi.

Ukarimbu wa Rama D na Jaydee ndo ulichangia kuzuka kwa uvumi huo. Rama Dee na Lady Dee wamewahi kutoa wimbo pamoja ‘Kama Huwezi’ uliotoka mwaka 2013.

Rama D na Lady Jaydee

Staa huyu alikana madai kuwa yeye na Jaydee ni wapenzi katika mahojiano na Bongo 5. Alisema yeye anamchukua Jaydee kama ndugu wake.

“Lady Jaydee unafahamu ni mtu ambaye kwanza naweza kusema ni mtu ni rafiki wa kweli alafu rafiki wa kawaida. Mimi nashangaa tu, tumeshibana, tumeelewana  muda wote tunaulizana, sehemu tuliokosea tunaulizana…urafiki wa namna hio yani. Sasa hivi umefikia nadhani kama ndugu yangu. Kwasababu kwa muda wowote naweza kumpigia simu tukazungumza,” Rama D alieleza.