Lord Eyes Afungukia Skendo Ya Mapenzi na Wolper

Msanii mkongwe wa muziki wa hop hop nchini kupokea katika kinda la Weusi Lord Eyes amefungukia tetesi zinazotrend kuwa Ana mahusiano na staa wa Bongo movie Jacqueline Wolper.

Kwa muda mfupi sasa kumekuwa na tetesi kuwa Lord Eyes na Wolper wamekuwa kwenye mahusiano hi ilitokana na picha kadhaa zilizowaonyesha wasanii hao pamoja.

Wiki iliyopita kwenye mahojiano yake na Global Publishers, Wolper alikataa tetesi hizo Lakini pia aliweka hao tatizo Kama ikitokea hivyo:

Unajua hata mimi ambaye naambiwa natoka naye nimeona kwenye mitandao tu lakini pia siku ikitokea, freshi tu.Sio mwanaume mbaya maana ana sifa zote za mwanaume ninayempenda au wamesema hivyo kwa sababu niliimba wimbo wake nikauposti mtandaoni ndio tatizo basi ngoja tuone itakavyokuwa maana Wabongo wape picha tu maneno wataweka wenyewe”.

Lakini pia Lord Eyes amefungukia tetesi hizo kwenye mahojiano na kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv na kusema habari hizo hazina Ukweli wowote:

Wolper ni radioing yangu tu na unajua maana ya rafiki ni mtu anayeweza kukusitiri na ndoto unamuita rafiki wa kweli”.

 

Wolper- Sioni Tatizo Kutoka na Lord Eyes

Mbunifu wa mavazi na muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa hana uhusiano na msanii mkongwe wa muziki wa Hip hop nchini Waziri Makuto maarufu kama Lord Eyes.

Kumekuwa na tetesi zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Wolper na Lord Eyes wapo kwenye mahusiano ya kimapenzi lakini Wolper amefungukia madai hayo na kusema kuwa hayana ukweli wowote.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Wolper  alisema yeye ameona kwenye mitandao taarifa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na Lord lakini pia hata siku ikitokea ikawa hivyo sio mbaya kwani sio mwanaume mbaya kwake na pia anavutiwa na jinsi alivyo.

Unajua hata mimi ambaye naambiwa natoka naye nimeona kwenye mitandao tu lakini pia siku ikitokea, freshi tu.Sio mwanaume mbaya maana ana sifa zote za mwanaume ninayempenda au wamesema hivyo kwa sababu niliimba wimbo wake nikauposti mtandaoni ndio tatizo basi ngoja tuone itakavyokuwa maana Wabongo wape picha tu maneno wataweka mwenyewe.”