“Hamisa Ndio Kiboko Ya Zari”- Maimartha

Mtangazaji mkongwe nchini Maimartha Wa Jesse amerudi tena kwenye headlines za mitandao ya kijamii Baada ya kutoa kauli tata ya Hamisa Mobetto dhidi ya Zarinah Hassan.

Siku mbili zilizopita mlimbwende Hamisa Mobetto alikuwa anasheherekea siku yake ya kuzaliwa na mmoja kati ya watu waliojitokeza kumtakia Birthday njema n Maimartha.

Maimartha Kupitia ukurasa wake wa Instagram alimuandikia ujumbe ambao ulizua maswali kwani alimuhusisha Mobetto na adui yake namba moja Zari ambapo aliandika maneno haya:

Happy Birthday Hamisa Kiboko ya Zari, ulijua kuwaparaganisha na Chibu…Zari alitamani akumeze ishi maisha dill yenye mafanikio”.

 

Maimartha Aongelea Kumuita Jokate Mama wa Taifa.

Mtangazaji na mc maarufu nchini Maimartha amefunguka na kuongelea  video iliyo-trend sana katika mitandao ya kijamii wiki iliyopita ikimuonyesha akiwa katika  hafla ya Zamaradi  akimuita jokate mama wa taifa swala lililozua sana mtafaruku katika mitandao.

Maimarha anasema kuwa swala la yeye kumuita Jokate hivyo ni kwa sababu Jokate amekuwa mwanamke wa kuigwa na wanawake wengine kutokana na kujitoa kwake katika jamii hasa baada ya kuwa akifanya mambo mengi ya kunufaisha jamii.

Jokate ni mwanamke, oate ni mfano wa kuigwa,nadhani nilichokisema hata mh magufuli kakiona  hicho kitu na kama mwanamke unapokuwa unajulikana tumia hiyo nafasi kuelimiesha wengine , hata kama unasema kiasi gani,haijalishi kwenye mahusiano yako uumekutana na changamoto gani.haijalishi umedondoka au umeanguka mara ngapi.she is a mom, ni mama na kuna ambao wameunganisha , Unaweza ukaiunganisha lakini  naomba wasinitafutie shida..