Majizo Aunda Kamati Ya Kusaidia Matibabu Ya Ruge

Mkurugenzi wa EFM na E-TV, Majizo ameunda kamati ambayo itaratibu namna ya kukusanya fedha za kusaidia mtibabu ya mkurugenzi wa vipindi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba ambaye yupo nchini Afrika Kusini kwa matibabu.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Cloud360 cha Clouds Tv, Majizzo amesema kuwa kamati ya kuchangisha wa pesa za matibabu imeshaundwa na imeanza kukutana siku ya jana.

Lengo letu ni moja tu kuhakikisha Ruge anarudi mtaani kwani gemu bila yeye linakuwa halina ushindani, Watanzania tunapokuja kwenu tunaomba mtupokee kwani Ruge ni wetu sote sio wa Clouds tu”.

Lakini pia Majjizo amekanusha tetesi za yeye na Ruge kuwa na bifu na kusema kuwa ni mtu ambaye amekuwa kama kaka, rafiki na mshauri kwake kwani ana mchango mkubwa kwake katika kufungua vituo vyake vya habari.

Hamisa Mobetto Awajia Juu Watu Wanaombeza Kisa Amezaa na Wanaume Wenye Hela

Muigizaji wa Bongo movie na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Haida Mobetto amewajia juu watu wanaombeza baada ya kusema kuwa yeye sio Single mothers.

Siku ya juzi ilikuwa ni Mother’s Day/ siku ya Mama duniani na Hamisa aliweka wazi kuwa yeye sio Single mother kwa sababu anasaidiwa kulea watoto wake na Baba watoto wake.

Hamisa ana watoto wawili ambapo mtoto wake wa kwanza Fantansy amezaa na Majizzo na mtoto wake wa pili Dylan amezaaa na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Lakini baada ya video hiyo kuingia mtandaoni watu walianza kumsema vibaya kutokana na yeye kuongelea suala lake la kuzaa na wanaume wawili tofauti ambao wote ameweka wazi wana uwezo.

Kupitia ukurasa wake wa Snapchat Hamisa altoa povu hili:

Mnatakiwa mjua kwamba Fancy na Dee Mungu ndo alipanga wazazi wa hawa watoto wawe nani..hasira zenu please msinimalizie mie mtoto wa marehemu Mzee hassan..Its getting boring now.”