Nahreel Afungukia Ishu Ya Rosa Ree Kuondoka The Industry

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka katika kundi la Navy Kenzo, Nahreel amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu msanii Rosa Ree kuondoka Kwenye label yake ya The Industry.

Msanii wa kike anayefanya vizuri kwa hivi sasa Rosa Ree alianza kujulikana baada ya kusainiwa chini ya label ya The Industry inayomilikiwa na Nahreel ambaye pia ni producer.

Rosa Ree alitangaza kuondoka kwenye label hiyo mapema mwaka jana baada ya kuwepo humo kwa muda mrefu huku akidai sababu pekee iliyomuondoa ni kuisha kwa mkataba wake na kusisitiza hana ubaya nao.

Lakini baadae Rosa Ree aliweka wazi kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo yalifanyika ndani ya label hiyo ambayo hayakumfurahisha ikiwemo kukataa kumpa akaunti yake ya Youtube hali iliyoashiria kulikuwa na kabifu fulani.

NAhreel anefunguka kwa mara ya kwanza na kumuongelea Rosa Ree tangu alipoondoka The Industry ambapo kwenye kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv ameweka wazi hakukuwa na bifu baina yao bali mwenyewe aliomba kuondoka.

Rosa Ree watu wamemjua Kupitia The Industry na kama alivyosema yeye time ilivyofika alitaka kuondoka na sisi tukamuacha aende but hatuna tatizo Rosa”.