Queen Vee na Calisah Wanasa Katika Penzi Zito.

Mwanamitindo mtanzania calisah anasemekana kunasa katika penzi zito na mwanadada kutoka uganda Queen vee ambae hivi karibuni alikuwa akilia kuteswa na mapenzi na mwanaume ambae alikuwa akimtumia kwa ajili ya jina lake na pia kutokana na pesa zake.

Wawili hao wanaoekana kuwa katika penzi jipya lakini pianwamekuwa wakishidwa kuficha mahaba hayo na kuitumia mitandao ya kijamii  kuanika mahusiano yao hadharani na mbele ya mashabiki.

Queen alikuwa na mahusiano na msanii Otile brown kwa muda mrefu kidogo lakini alikuja kulalamika hadharani kuwa mwanaume huyo amekuwa akimtumia kwa ajili ya mambo yake binafsi ya kujinufaisha kimuziki na kimaisha pia.