Kundi la Rich Gang yamwaga pombe na kutupa pesa kwenye kaburi la Ivan Ssemwanga (Video)

Ivan Ssemwanga alikuwa mwanzilishi wa kundi la Rich Gang ambalo ni maarufu sana nchini Uganda kwa kufanya party za nguvu. Wanachama wa kundi hilo ni matajiri wakubwa ambao wanapenda sana maisha ya anasa.

Rich Gang walifanya ibada yao maalum kwenye kaburi la Ivan baada ya kanisa kufanya ibada ya maombi. Wanachama wa Rich Gang waliizingiza kaburi la mwanzilishi wao na kumwaga pombe ndani na pia kutupa pesa ndani la kaburi hilo.

Hii ilikua kabla ya jeneza la Ivan kuteremshwa kwenye kaburi lake. Waombolezaji waliskika wakishangilia wanachama wa Rich Gang walipokua wakitupa pesa kwenye kaburi la Ivan.

Tamaza video hapo chini:

https://www.youtube.com/watch?v=nNtSSzHPZjY