Aikah Afunguka Kuhamia WCB

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Kutoka katika kundi la Navy Kenzo Aikah Marealle amefunguka na kuongolea taarifa za kuhamia WCB.

Baada ya kutoa hit single ambayo inaendelea kufanya vyema mpaka sasa ‘Katika’ waliomshirikisha Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz kuliibuka tetesi kuwa Nahreel na Aika wamehamia chini ya WCB.

Kwenye mahojiano yake na Global Publishers , Aika  amesema kuwa, amekuwa akisikia kwa watu wengi juu ya kuhamia WCB mara baada ya kuachia wimbo wao  na Diamond jambo ambalo halina ukweli.

Yaani watu wengi wanasema nimehamia WCB lakini ukweli ni kwamba tuna meneja anayetokea huko anaitwa Sallam na amekuwa akitusimamia sasa sijui hayo mengine yanatokea wapi.

Nilikaa na mwenzangu tukatunga Wimbo wa Katika tukaona ni vizuri tukamshirikisha Diamond ndiyo ikawa hivyo sasa nashangaa hao wanaoungaunga maneno”.

Tetesi hizo za Kuhamia WCB zilipamba moto mara baada ya Msanii kutoka WCB Harmonize kusema wazi kuwa wasanii hao wanahamia Kwenye Label yao taarifa ambazo Navykenzo walidai ulikuwa ni utani.

Mameneja Wa Diamond Wadaiwa Kuhusika na Kusambaza Video Ya Ngono Ya Nandy

Kama utakumbuka mwezi uliopita jiji zima lilizizima baada ya video ya ngono iliyomuhusisha msanii wa Bongo fleva Nandy na Billnas kusambaa kwenye mitandao ya kijamii na kusababisha skendo kubwa kwa wasanii hao.

Chanzo cha video hiyo hakikujulikana kwa sababu Nandy na Billnas wote walikataa kuhusika na kusambazwa kwa video hiyo lakini aliyeiweka video hiyo Mtandaoni ni kurasa ya Udaku inayojulikana kama UdakuTz.

Sasa tangu wikiendi iliyopita kuna taarifa zilizodai kuwa mmiliki wa kurasa hiyo ya udaku ametekwa na watu wasiojulikana kwani familia yake haijui alipo, mpaka jana ambapo ilidaiwa alichukuliwa na polisi kwa ajili ya mahojiano juu ya kuvuja wa  video ile ya Nandy na Billnas.

Lakini taarifa iliyotolewa jana na mtangazaji wa Clouds Fm Soudy Brown ni kuwa mmiliki wa kurasa hiyo yupo kituo cha polisi na Kwenye mahojiano hayo amewataja watu waliompa video hiyo avujishe ambao walikuwa ni mameneja wa Diamond ambao mi Salaam SK na Babu Tale.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Soudy Brown aliweka posti hii:

Mpaka sasa haijajulikana kama Watajwa hapo juu  ambao wote ni mameneja wa Diamond wameshatiwa mbaroni au bado.

Lakini pia haijawekwa wazi ni vipi Msanii Diamond anahusika vipi katika hilo lakini yote hii inarudi katika bifu la Diamond na Clouds Media.