Sister Fey Amfungukia Mazito Hamisa Mobetto

Msanii wa Bongo fleva Faidha Omary maarufu kwenye mitandao ya kijamii Kama Sister Fey ameibuka na kumpa maneno mazito Mwanamitindo Hamisa Mobetto.

Sister Fey amemuibukia Hamisa na Kumpongeza kwa mambo mazuri anayofanya hivi sasa nchini Marekani ambapo anafanya shoo mbali mbali katika nini mbali mbali.

Sista Fey amemtaka kuwa jasiri na kutoangalia nyuma sasa kwani alipotoka ni mbali lakini alipofika hivi sasa ni mbali zaidi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Sista Fey ameandika maneno haya:

Uanawza ukatukanwa Sana na ukadhalilishwa sana ukapitia magunu mpaka ukajiuliza kwanini Mimi? ILA siku ni moja tu kila mmoja atashangaa hata maadui zako watajificha kukuangalia kimya kimya wakati wa Mungu ni wakati sahihi but Hamisa nakuomba na kukuombea usirudi nyuma ikiwezekana kweli chukua uraia huko na ikishindikana piga kazi haswa hakikisha unapata madili mengi ili uzidi kuwanyamazisha wabaya wako Misa dunia dura mama na sitamani kusikia utoto umekurudisha nyuma kwa uliyopitia jione una miaka 40 wewe ni mrembo”.

 

Hamisa tangu ameachana na Diamond na kuelekeza nguvu zake kwenye kupiga kazi ameonekana kufanya vizuri na kufika mbali zaidi.

Sista Fey Amtolea Uvivu Steve Nyerere

Msanii wa Bongo movie Faidha Omary maarufu kama Sista Fey amemjia juu msanii mwenzake Steve Nyerere na kumuita mnafiki huku akimtuhumu kwa kusababisha mpaka yeye kukamatwa na kuwekwa ndani.

Sista Fey alikamatwa wiki chache zilizopita kutokana na kudaiwa kuanika maudhui mabaya kwenye mitandao ya kijamii lakini hivi sasa ameibuka na kumnyooshea kidole Steve Nyerere kama mtu aliyesababisha hayo yote.

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari, Sista Fey alimwaga povu hili;

Hapa Tanzania hakuna msanii mnafiki kama Steve Nyerere kwani anakusema asubuhi jioni anajifanya rafiki yako ila namuombe kwa Mungu aendelee na unafiki wake na hivyo anavyojifanya mwema kumbe mnafiki tu”.

Steve anajifanya kimbele mbele zaidi ya viongozi wetu halafu mimi kama Fey najua hakuna nilichokukosea ila roho yako mbaya uliyotengeneza kwanini mimi nionekane sana Instagram kuliko wewe itakugharimu kwani kila mwanaadamu ana karama yake wewe karama yako kuiga sauti za viongozi wewe sio kiongozi”.

 

Sista Fey Awekwa Ndani Kwa Amri Ya Naibu Waziri

Muigizaji wa Bongo movie na msanii wa Bongo fleva Faidha Omary maarufu kama Sista Fey amejikuta katika upande mbaya wa sheria baada ya kuwekwa rumande.

Sista Fey yupo chini ya ulinzi kufuatia tabia yake ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ambayo imempa umaarufu mkubwa na kujulikana na watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii.

Sista Fay na mpenzi wake ambaye pia ni msanii Hollystar walijizolea umaarufu baada ya kuposti video mbali mbali ambazo ziliangaliwa kama kuwa ni kinyume na maadili ya Kitanzania.

Taarifa ya kuwekwa chini ya ulinzi imetolewa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo ameandika:

 

Kibenten Champonza Sista Fey Atimuliwa Kwenye Nyumba Ya Kupanga

Msanii wa Bongo fleva na bongo movie Faiza Omary  Maarufu kama Sista Fey amejikuta akitimuliwa Kwenye Nyumba aliyokuwa anaishi baada ya video na kibenten chake kusambaa mitandaoni.

Sista Fey na mpenzi wake Holly Star wamejizolea umaarufu Kwenye mitandao ya kijamii baada ya video zao kusambaa Lakini pia hilo limekuwa tatizo kwani wametimuliwa Kwenye Nyumba waliokuwa wanaishi.

Global Publishers wanaripoti kuwa Mwanzoni Fey hakuwa na kibenten wake huyo, lakini baada ya muda ndiyo akampeleka wakawa wanaishi wote ila mama mwenye nyumba alikuwa akikereka na maisha wanayoishi kwa kuwa kuna wakati wanabebana na kupelekana bafuni, jambo ambalo aliona siyo zuri kwa watoto wanaoishi kwenye nyumba hiyo.

Baada ya Tetesi hizo gazeti hilo lilimsaka Fey ili kutaka kujua ukweli wa jambo hilo ambapo alifunguka:

Unajua mimi ni mkweli sana, kwenye hilo siwezi kukataa, ni kweli nimepewa barua, lakini nimepokea kwa mikono miwili maana huyu (Eliasi) ndiye nimempenda. Mambo aliyoandika mama mwenye nyumba kwenye barua ni ya kawaida kwa wapenzi”.

Lakini pia Fey amesisitiza kuwa wana mpango wa kufunga ndoa na kibenten chake:

Baada ya kuzungumza na Sister Fey, Ijumaa Wikienda lilimgeukia jamaa huyo ili naye afunguke madai ya kumsababishia Fey kupewa barua ya kuhamishwa kwenye nyumba ambapo alisema yeye haoni kama kuna tatizo kwenye hilo ila inawezekana hapo hawakuwapenda tu”.