Snura awajibu mashabiki wanaodhani anatumia dawa za kulevya Kabla ya kujibwaga jukwani

Kama ushawahi kumuona Snura akitumbuiza kwenye jukwaa, basi unaelewa kuwa yeye ni msanii ambaye huwaacha mashabiki wake kama wameridhika.

Lakini, kuna tetesi kuwa yeye hutumia pombe ili kutoa aibu ya kuwatumbuiza mashabiki wake. Hata hivyo hivi karibuni alifunguka kukana maneno haya.

Kulingana na yeye, hatumii pombe wala sigara jumps nguvu ya kutumbuiza. Alikiambia kipindi cha E-Newz ya EATV,

“Mimi napanda kwenye stage situmii kinywaji cha aina yoyote Mungu wangu aliyekamili ni shahidi. Sinywi pombe, sivuti na ninapanda kwenye stage ninahamsha kiasi kwamba unaweza kuhisi kuna kitu nimetumia kichwani, akili yangu nimeijenga hii ni kazi, huwezi kuona aibu kwa sababu ndio kazi uliyoichagua,”

Aliongeza,

“Kwa hiyo napenda nipande kwenye stage nikiwa mzima timamu nione kwa sababu hii ni kazi yangu naifanya, pia nafanya research kujua style gani nikicheza watu wananishangilia, wimbo gani nikiimba watu wanapenda,”

Snura akana kupangiwa nyumba na mwanaume wa Kiarabu

Inasemekana kuwa mwanamziki Snura amepangiwa nyumba mpya na mwanaume wa Kiarabua ambaye anaweza kuwa mpenzi wake hivi sasa.

Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa Global Publishers amabao walimtembelea katika nyumba yake huko maeneo ya Tabata, Dar Snura alikana kwa kusema kuwa hana mawanume wa kiarabu ambaye amempangia nyumba.

Aliendelea kusema kuwa alihamia sehemu hiyo ili mwanae awache kuchoka akienda shule. Hivi ndivyo mazungumzo yao yalikuwa.

Snura
Snura

Wikienda: Snura mambo vipi? Mbona kimya sana kimuziki? Au ndiyo mambo ya ubuyu unaosemwa?

Snura: Yapi tena? Mimi mbona nipo najiandaa kutoa kazi? Siyo kila siku kusikika bila mpango. Mimi huwa nasikika kwa kazi ninayoitoa ninyi subirini mtanisikia.

Wikienda: Hata hivyo, tuna ubuyu hapa kuwa nyumba hii umepangishiwa na mwanaume wa Kiarabu ambaye amekuhamisha Mwananyamala kwa sababu alikuwa hapapendi, unalizungumziaje hilo?

Snura: Hahahahaha, mmenichekesha kweli, watu wanajua kuongea sana, mimi nimehama nyumba kwa sababu ya mtoto. Shule anayosoma mwanangu ipo huku Tabata. Mwananyamala ilikuwa ni mbali sana. Mwanangu alikuwa anachoka sana. Hayo mengine ya mwanaume wa Kiarabu ndiyo kwanza nayasikia kwenu.

Wikienda: Nasikia amekununulia na gari la kutembelea maana tunaliona hapa, tunasikia ana mpango wa kukupiga stop kuimba, je, ni kweli?

Snura: Gari nimenunua mwenyewe kwa jasho langu nikimaanisha kazi yangu, huyo Mwarabu mnayemkazania kama yupo hakuna la kufi cha kwani mwisho wa yote atajulikana tu na ataonekana, lakini nahisi labda wanayemzungumzia ni baba mtoto wangu, hahaha…